Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu Gani Wakristo wa Kweli Hawatumii Musalaba Katika Ibada?

Sababu Gani Wakristo wa Kweli Hawatumii Musalaba Katika Ibada?

NYONGEZA

Sababu Gani Wakristo wa Kweli Hawatumii Musalaba Katika Ibada?

MAMILIONI ya watu wanaheshimu musalaba na wanauabudu. Kitabu kimoja (The Encyclopædia Britannica) kinasema kama musalaba ni “alama ya kwanza inayoonyesha dini ya Kikristo.” Lakini, Wakristo wa kweli hawatumii musalaba katika ibada. Kwa sababu gani?

Sababu ya kwanza ni hii: Yesu Kristo hakufa kwenye musalaba. Mara nyingi neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘musalaba’ ni stau·rosʹ. Neno hilo linamaanisha “muti ao nguzo iliyo wima.” Biblia moja (The Companion Bible) inasema hivi: “[Neno stau·rosʹ] halimaanishi hata kidogo vipande viwili vya mbao vilivyokingamana . . . Katika [Agano Jipya] hakuna neno lolote lililoandikwa katika luga ya Kigiriki linalotokeza wazo la vipande viwili vya mbao.”

Katika maandiko mengi, waandikaji wa Biblia wanatumia neno lingine ili kuonyesha chombo walichotumia ili kumutundika Yesu. Ni neno xyʹlon katika Kigiriki. (Matendo 5:30; 10:39; 13:29; Wagalatia 3:13; 1 Petro 2:24) Neno hilo linamaanisha tu “mbao” ao “kijiti ao muti.”

Ili kuonyesha kwa nini mara nyingi walikuwa wakitumia muti tu wa kawaida ili kuwatundika watu waliohukumiwa kifo, kitabu Das Kreuz und die Kreuzigung (La Croix et la Crucifixion) kilichoandikwa na Hermann Fulda, kinasema hivi: “Miti haikupatikana kila mahali ambapo palichaguliwa ili kuwatundikia watu waliohukumiwa kifo. Kwa hiyo, nguzo zilishimikwa katika udongo. Mara nyingi watenda mabaya walitundikwa kwenye nguzo hizo, mikono yao ilikuwa ikiinuliwa juu na mara nyingi miguu yao ilikuwa ikifungwa ao kupigiliwa misumari.”

Hata hivyo, sababu inayotoka katika Neno la Mungu ndio inayosadikisha zaidi kuliko sababu zingine zote. Mutume Paulo alisema hivi: ‘Kristo kwa kutununua alituachilia huru kutoka katika laana ya Sheria kwa yeye kuwa laana badala yetu, kwa sababu imeandikwa: Amelaaniwa kila mutu aliyetundikwa juu ya muti.’ (Wagalatia 3:13) Hapa Paulo anarudilia andiko la Kumbukumbu la Torati 21:22, 23, ambalo linazungumuzia waziwazi muti, wala si musalaba. Kwa sababu watu waliotundikwa hivyo walionekana kuwa “laana,” haifai Wakristo kupamba nyumba zao kwa sanamu za Kristo mwenye kutundikwa juu ya muti wa mateso.

Hakuna ushuhuda wowote unaoonyesha kama kwa muda wa miaka 300 kisha kufa kwa Kristo, wale waliojiita Wakristo walitumia musalaba katika ibada. Hata hivyo, katika miaka ya 300 hivi, mutawala mupagani Constantin alijiunga na Wakristo waasi-imani na kusema kama musalaba ndiyo alama yao. Hata iwe ni nini iliyomusukuma Constantin kusema hivyo, jambo la maana ni kama musalaba haukuwa na uhusiano wowote na Yesu Kristo. Kwa kweli, musalaba una chanzo cha kipagani. Kitabu kimoja (New Catholic Encyclopedia) kinasema hivi: “Musalaba ulitumiwa na watu walioishi mbele ya Yesu kuzaliwa na watu ambao hawakuwa Wakristo.” Watu fulani wenye kujulikana sana wamesema kama musalaba ulitumiwa katika ibada ya viumbe na desturi za kipagani za ngono.

Basi, kwa nini alama hiyo ya kipagani ilienezwa? Inaonekana kama ilienezwa ili kufanya iwe vyepesi kwa wapagani kukubali Ukristo wa uongo. Lakini, Biblia inalaumu waziwazi kushikamana na alama yoyote ya kipagani. (2 Wakorintho 6:14-18) Biblia inakataza pia kila namna ya ibada ya sanamu. (Kutoka 20:4, 5; 1 Wakorintho 10:14) Kwa hiyo, Wakristo wa kweli wana haki ya kukataa kutumia musalaba katika ibada. *

[Maelezo ya chini]

^ fu. 5 Ili kupata maelezo zaidi juu ya musalaba, soma kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, ukurasa wa 211-215, chapa ya 2004, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.