Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1914​—Ni Mwaka wa Maana Sana Katika Unabii wa Biblia

1914​—Ni Mwaka wa Maana Sana Katika Unabii wa Biblia

NYONGEZA

1914​—Ni Mwaka wa Maana Sana Katika Unabii wa Biblia

MIAKA 40 hivi mbele ya mwaka wa 1914, wanafunzi wa Biblia walitangaza kama matukio ya maana yangetokea mwaka wa 1914. Ni matukio gani hayo, na ni nini iliyoonyesha kama mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka wa maana sana?

Katika andiko la Luka 21:24, Yesu alisema hivi: ‘Yerusalemu itakanyagwa-kanyagwa na mataifa, mupaka nyakati zilizowekwa za mataifa zitimie.’ Yerusalemu ulikuwa muji mukubwa wa taifa la Wayahudi​—kiti cha utawala cha kizazi cha wafalme wa nyumba ya mufalme Daudi. (Zaburi 48:1, 2) Wafalme hao walikuwa tofauti na viongozi wa mataifa mengine. Wao waliketi kwenye “kiti cha ufalme cha Yehova,” ni kusema, walitawala mahali pa Mungu mwenyewe. (1 Mambo ya Nyakati 29:23) Kwa hiyo, Yerusalemu ilifananisha utawala wa Yehova.

Basi, ni namna gani na ni wakati gani utawala wa Mungu ulianza ‘kukanyagwa-kanyagwa na mataifa’? Jambo hilo lilianza mwaka wa 607 mbele ya Yesu kuzaliwa, wakati majeshi ya Babiloni yaliharibu Yerusalemu. Kuanzia wakati huo hakuna mutu aliyeketi kwenye “kiti cha ufalme cha Yehova,” na kizazi cha wafalme wa uzao wa Daudi kilikatizwa. (2 Wafalme 25:1-26) Je, Yerusalemu ‘ingekanyagwa-kanyagwa’ milele? Hapana, kwa sababu unabii ambao Ezekieli alitoa juu ya Sedekia, mufalme wa mwisho wa Yerusalemu, ulisema hivi: ‘Kiondoe kilemba, na kulivua taji. Hakika hili halitakuwa la mutu yeyote mupaka atakapokuja yule aliye na haki ya kisheria, nami nitamupa yeye.’ (Ezekieli 21:26, 27) Kristo Yesu ndiye aliye na “haki ya kisheria” ya kuvaa taji la Daudi. (Luka 1:32, 33) Kwa hiyo, ‘kukanyagwa-kanyagwa’ kungeisha wakati ambapo Yesu angekuwa Mufalme.

Jambo hilo kubwa lingetokea wakati gani? Yesu alionyesha kama Mataifa yangetawala kwa wakati fulani uliowekwa. Habari iliyo katika Danieli sura ya 4 inatusaidia kujua urefu wa wakati huo. Inazungumuzia ndoto ya kiunabii ambayo Mufalme Nebukadneza wa Babiloni aliota. Aliona muti mukubwa uliokatwa. Kisiki chake hakingeweza kuota kwa sababu kilikuwa kimefungwa kwa pingu ya chuma na ya shaba. Malaika alitangaza hivi: “Nyakati saba zipite juu yake.”​—Danieli 4:10-16.

Katika Biblia, kuna wakati miti inafananisha utawala. (Ezekieli 17:22-24; 31:2-5) Kwa hiyo, kukatwa kwa muti huo wa mufano kunaonyesha namna utawala wa Mungu, uliofananishwa na utawala wa wafalme wa Yerusalemu, ungekatizwa. Hata hivyo, ndoto hiyo ilionyesha pia kama ‘kukanyagwa-kanyagwa kwa Yerusalemu’ kulipaswa kuwa kwa muda, yaani, kipindi cha “nyakati saba.” Kipindi hicho kilipaswa kuchukua muda gani?

Andiko la Ufunuo 12:6, 14 linaonyesha kama nyakati tatu na nusu zinalingana na “siku 1260.” Kwa hiyo, “nyakati saba” zilipaswa kuchukua muda wa siku 1260 mara mbili, ni kusema, siku 2520. Lakini, siku 2520 tu kisha kuharibiwa kwa Yerusalemu, Mataifa hayakuacha ‘kukanyaga-kanyaga’ utawala wa Mungu. Kwa hiyo, inaonekana wazi kama unabii huo ulizungumuzia muda murefu zaidi. Kupatana na maneno yaliyo katika Hesabu 14:34 na Ezekieli 4:6, siku moja inachukuliwa kama mwaka moja. Hesabu hiyo inasaidia kujua kama zile “nyakati saba” zingekuwa miaka 2520.

Miaka hiyo 2520 ilianza mwezi wa kumi mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, wakati majeshi ya Babiloni yalichukua Yerusalemu na kuondoa mufalme wa uzao wa Daudi kwenye kiti cha ufalme. Kipindi hicho kilimalizika mwezi wa kumi mwaka wa 1914. Wakati huo, “nyakati zilizowekwa za mataifa” zilimalizika, na Yesu Kristo akawekwa kuwa Mufalme aliyechaguliwa na Mungu huko mbinguni. *​—Zaburi 2:1-6; Danieli 7:13, 14.

Kama Yesu alivyotabiri, matukio ya pekee duniani, kama vile, vita, njaa, matetemeko ya inchi, magonjwa ya kuambukiza, yanaonyesha “kuwapo” kwa Yesu na kama yeye ametiwa kuwa Mufalme mbinguni. (Mathayo 24:3-8; Luka 21:11) Matukio hayo yanaonyesha wazi kama Ufalme wa mbinguni wa Mungu ulizaliwa mwaka wa 1914 na kama “siku za mwisho” za ulimwengu huu muovu zilianza mwaka huo.​—2 Timotheo 3:1-5.

[Maelezo ya chini]

^ fu. 3 Kuanzia mwezi wa kumi mwaka wa 607 kabla ya wakati wetu mupaka mwezi wa kumi mwaka wa 1 kabla ya wakati wetu ni miaka 606. Hakuna mwaka zero. Kuanzia mwezi wa kumi mwaka wa 1 wakati wetu mupaka mwezi wa kumi mwaka wa 1914 ni miaka 1914. Tukikamata miaka 606 na kuongeza miaka 1914, tunapata miaka 2520. Ili kupata maelezo zaidi juu ya kuharibiwa kwa Yerusalemu katika mwaka wa 607, soma habari “Chronologie” katika kitabu Étude perspicace des Écritures, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.