Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Malaika Mukubwa Anayeitwa Mikaeli Ni Nani?

Malaika Mukubwa Anayeitwa Mikaeli Ni Nani?

NYONGEZA

Malaika Mukubwa Anayeitwa Mikaeli Ni Nani?

BIBLIA haisemi mara nyingi juu ya Mikaeli. Lakini, inapomutaja Mikaeli, wakati huo yeye ni mwenye kufanya jambo fulani. Kwa mufano, katika kitabu cha Danieli, Mikaeli anapigana na malaika wabaya; katika barua ya Yuda, anabishana na Shetani; na katika Ufunuo, anapigana na Ibilisi na mashetani wake. Kwa sababu Mikaeli anatetea utawala wa Yehova na anapigana na adui za Mungu, hilo linaonyesha kama anatenda kulingana na maana ya jina lake, yaani, “Ni Nani Aliye Kama Mungu?” Kwa hiyo, Mikaeli ni nani kabisa?

Wakati mwingine, mutu anaweza kuwa na majina mengi. Kwa mufano, Yakobo muzee wa ukoo aliitwa pia Israeli, na mutume Petro aliitwa Simoni. (Mwanzo 49:1, 2; Mathayo 10:2) Kwa hiyo, Biblia pia inaonyesha kama Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo, mbele ya yeye kuja duniani na kisha kurudi mbinguni. Acha tuone Maandiko yanayoonyesha jambo hilo.

Malaika Mukubwa. Neno la Mungu linamuita Mikaeli ‘malaika mukubwa.’ (Yuda 9) Hilo linamaanisha kama Mikaeli ndiye mukubwa wa malaika na ni mumoja tu. Tena, katika Biblia, jina ‘malaika mukubwa’ linatumiwa katika hali ya umoja tu (singulier), wala si ya uwingi (pluriel). Zaidi ya hayo, wanapotaja cheo cha malaika mukubwa mara moja watu wanawaza juu ya Yesu. Andiko la 1 Wathesalonike 4:16 linazungumuza juu ya Bwana Yesu Kristo aliyefufuliwa, linasema hivi: ‘Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mukubwa.’ Hapa, sauti ya Yesu inasemwa kuwa sauti ya malaika mukubwa. Kwa hiyo, andiko hilo linaonyesha kama Yesu mwenyewe ndiye Mikaeli yule malaika mukubwa.

Kiongozi wa Jeshi. Biblia inasema kama ‘Mikaeli na malaika zake walipigana na yule joka mukubwa na malaika zake.’ (Ufunuo 12:7) Kwa hiyo, Mikaeli ni Kiongozi wa jeshi la malaika waaminifu. Tena, kitabu cha Ufunuo kinamutaja Yesu kuwa Kiongozi wa jeshi la malaika waaminifu. (Ufunuo 19:14-16) Na mutume Paulo anamutaja waziwazi “Bwana Yesu” na “malaika zake wenye nguvu.” (2 Wathesalonike 1:7) Biblia inapozungumuza juu ya Yesu inatumia maneno Mikaeli na “malaika zake” pia Yesu na “malaika zake.” (Mathayo 13:41; 16:27; 24:31; 1 Petro 3:22) Kwa sababu katika Neno la Mungu hakuna andiko linaloonyesha kama kuna majeshi mawili ya malaika waaminifu mbinguni, kama jeshi moja linaongozwa na Mikaeli na lingine linaongozwa na Yesu, hilo linaonyesha wazi kama Mikaeli si mwingine ila ni Yesu Kristo akiwa katika cheo chake huko mbinguni. *

[Maelezo ya chini]

^ fu. 1 Ili kupata maelezo zaidi yanayoonyesha kama jina Mikaeli ni la Mwana wa Mungu, soma kitabu Étude perspicace des Écritures Buku la 2, ukurasa wa 280-281, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.