Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Ni Vibaya Kufanya Sikukuu?

Je, Ni Vibaya Kufanya Sikukuu?

NYONGEZA

Je, Ni Vibaya Kufanya Sikukuu?

KATIKA sehemu nyingi za dunia, sikukuu nyingi ambazo watu wanapenda kufanya leo, iwe ni za kidini ao hapana, hazitokani na Biblia. Basi, sikukuu hizo zilianzia wapi? Ikiwa unapata nafasi ya kuingia katika maktaba (mahali pa kuwekea vitabu ili watu wavisome ao waviazime) fulani utashangaa kusoma mambo ambayo vitabu vingine vinasema juu ya sikukuu zinazofanywa na watu wengi mahali unapoishi. Acha tuchukue mifano fulani.

Sikukuu ya Pasaka (Pâques). Kitabu kimoja (The Encyclopædia Britannica) kinasema hivi: “Katika Agano Jipya, hakuna mahali panapoonyesha kama Wakristo walikuwa wakifanya sikukuu ya Pasaka.” Sikukuu hiyo ilianza namna gani? Imetokana na ibada ya kipagani. Ijapokuwa inasemekana kama sikukuu hiyo ni ukumbusho wa kufufuka kwa Yesu, desturi za watu kwenye sikukuu ya Pasaka si za Kikristo. Kwa mufano, kitabu kimoja (The Catholic Encyclopedia) kinasema hivi juu ya yule “sungura wa Pasaka,” alama inayotumiwa na watu wengi: “Sungura huyo ni alama ya kipagani ambayo sikuzote inaonyesha nguvu za uzazi.”

Sikukuu ya Mwaka Mupya. Tarehe na desturi za watu juu ya Sikukuu ya Mwaka Mupya zinatofuatiana katika inchi mbalimbali. Kitabu kimoja (The World Book Encyclopedia) kinasema hivi juu ya chanzo cha sikukuu hiyo: “Katika mwaka wa 46 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Mutawala Muroma Jules César alitia sheria inayosema kama tarehe 1 mwezi wa kwanza ni Siku ya Mwaka Mupya. Waroma walikuwa tayari wanafanya sikukuu hiyo kwa ajili ya Janus, mungu wa milango, na wa mwanzo wa mambo. Jina la mwezi wa kwanza, yaani Janvier, lilitokana na jina la mungu huyo Janus, aliyekuwa na nyuso mbili​—uso moja uliangalia mbele na mwingine uliangalia nyuma.” Kwa hiyo, sherehe za Mwaka Mupya zinatokana na desturi za kipagani.

Sikukuu ya Watakatifu Wote (Halloween). Kitabu kimoja (The Encyclopedia Americana) kinasema hivi: “Desturi fulani-fulani zinazohusiana na Sikukuu ya Watakatifu Wote zilitokana na sherehe za kidini za Kiselti za mbele ya Ukristo. Waselti walikuwa na sikukuu kwa ajili ya miungu wawili wakubwa, yaani, mungu-jua na mungu wa watu waliokufa . . . , ambaye sikukuu yake ilikuwa ikifanywa tarehe 1 mwezi wa kumi na moja, mwanzo wa Mwaka Mupya wa Kiselti. Polepole, sikukuu hiyo ya watu waliokufa ikaingizwa katika desturi za Kikristo.”

Sikukuu Zingine. Haiwezikani kuzungumuzia kila sikukuu inayofanywa duniani pote. Hata hivyo, sikukuu zinazowatukuza wanadamu ao mashirika ya kibinadamu hazimupendezi Yehova. (Yeremia 17:5-7; Matendo 10:25, 26) Tena, kumbuka kama namna sikukuu fulani ya kidini ilivyoanza ndio inaweza kufanya sikukuu hiyo imupendeze Mungu ao imuchukize. (Isaya 52:11; Ufunuo 18:4) Kanuni za Biblia zilizotajwa katika Sura ya 16 zitakusaidia kujua maoni ya Mungu juu ya sikukuu zisizo za kidini.