Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Yosefu

Mfano wa Kuigwa—Yosefu

Mfano wa Kuigwa—Yosefu

Yosefu anakabili hali ngumu. Mke wa bwana wake amemsihi tena na tena afanye ngono naye. Sasa anajaribu tena! Lakini Yosefu anakataa. Anajibu kwa uthabiti. Anamwambia: “Ninawezaje kufanya ubaya huu mkubwa na kwa kweli nimtendee Mungu dhambi?” Mwanamke huyo anaposisitiza—hata kwa kumshi­ka—Yosefu haoni haya kukimbia. Anakimbia na kwenda nje! Yosefu anathibitisha kwamba ni mshikamanifu kiadili.Mwanzo 39:7-12.

Wewe pia unaweza kujikuta katika hali kama hiyo ambayo mtu anataka utosheleze tamaa zako za ngono. Hutakataa tu kwa sababu unaweza kujidhibiti. Lakini utakataa kwa sababu unataka kumpendeza Muumba wako, Yehova Mungu. Yosefu alikuwa na tamaa za ngono, kama wewe. Hata hivyo, lilikuwa jambo lisilowazika kwake kutosheleza tamaa hizo kwa njia ambayo ingemkasirisha Muumba wake. Kwa njia hiyohiyo, unapaswa kusadiki kwamba uchafu wa kiadili unamkasirisha Mungu na mwishowe unaleta maumivu makali. Kwa hiyo, jitahidi kukuza na kudumisha ushikamanifu wa kiadili kama Yosefu alivyofanya.