Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Yule Mjane Maskini

Mfano wa Kuigwa—Yule Mjane Maskini

Mfano wa Kuigwa—Yule Mjane Maskini

Yesu anawatazama matajiri wakitumbukiza michango ndani ya sanduku la hazina hekaluni. Katikati ya umati huo, anamwona mjane mmoja mwenye uhitaji ambaye anatoa “sarafu ndogo mbili za thamani ndogo sana.” (Luka 21:2) Yesu anamsifu kwa sababu ya tendo hilo la ukarimu. Kwa nini? Kwa sababu wengine walikuwa wametoa “kutokana na ziada yao, lakini yeye, kutokana na uhitaji wake, alitumbukiza ndani vyote alivyokuwa navyo, riziki yake yote.”Marko 12:44.

Je, unatanguliza mambo ya maana kama mwanamke huyo alivyofanya? Je, uko tayari kutumia wakati na pesa zako kumtumikia Yehova? Kama mjane huyo, unaweza kutoa mchango kwa ajili ya udumishaji wa mahali pa ibada. Pia, unaweza kutumia wakati na pesa zako kuwafundisha wengine kumhusu Yehova Mungu. Yehova aliona na kuthamini kiasi kidogo ambacho yule mjane alitoa kwa ajili ya utumishi wake. Mungu atathamini na atakusaidia pia ikiwa unatanguliza kufanya mapenzi yale.—Mathayo 6:33.