Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Paulo

Mfano wa Kuigwa—Paulo

Mfano wa Kuigwa—Paulo

Mtume Paulo anaelewa vizuri hisia zake. Anakiri hivi waziwazi: “Ninapotaka kufanya yaliyo sawa, yaliyo mabaya yapo pamoja nami.” Paulo ana moyo mzuri. Anasema: “Kwa kweli naipenda sheria ya Mungu kulingana na mtu niliye kwa ndani.” Shida ni nini basi? Paulo anasema: “Naona . . . sheria nyingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya dhambi iliyo ndani ya viungo vyangu.” Paulo hafurahii kuwa katika hali hiyo. Anasema hivi kwa majuto: “Maskini mimi!”—Waroma 7:21-24.

Je, wewe huvunjika moyo kwa sababu ya makosa unayofanya? Ikiwa ndivyo, kumbuka kwamba hata Paulo alihisi hivyo nyakati fulani. Lakini Paulo alijua kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya watu kama yeye. Hivyo, angeweza kusema: “Shukrani kwa Mungu kupitia Yesu Kristo Bwana wetu!” (Waroma 7:25) Paulo aliiona fidia kuwa zawadi yake binafsi. Aliandika: ‘Mwana wa Mungu, alinipenda mimi na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.’ (Wagalatia 2:20) Unaposhuka moyo, tafakari kuhusu fidia. Na ikiwa makosa yako yanakuvunja moyo, usisahau kamwe kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya wakosaji, bali si watu wakamilifu.