Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 12

‘Kusema Bila Woga kwa Mamlaka ya Yehova’

‘Kusema Bila Woga kwa Mamlaka ya Yehova’

Paulo na Barnaba walionyesha unyenyekevu, uvumilivu, na uhodari

Inategemea Matendo 14:1-28

1, 2. Ni mambo gani inatokea wakati Paulo na Barnaba wako Listra?

 MU MUJI wa Listra muko muvurugo sana. Mwanaume mwenye alizaliwa kilema anaruka kwa furaha kisha wanaume wawili wenye hajue kumuponyesha. Watu wanashangala sana na kuhani analeta mataji ya maua kwa ajili ya wale wanaume wawili wenye watu wanaona kuwa miungu. Ngombe dume wanapumua nguvu sana na kufanya makelele wakati kuhani wa Zeu iko najitayarisha ili kuwatoa zabihu. Paulo na Barnaba wanakataza watu wasifanye vile. Wanapasua nguo zao na wanaingia katikati ya watu wengi na kuwaomba wasiwaabudu. Inaomba wafanye nguvu yao yote ili wakataze watu.

2 Kisha, Wayahudi wapinzani wanafika kutoka Antiokia ya Pisidia na Ikoniamu. Wanasemea Paulo na Barnaba uongo na wanafikia kushawishi watu wa Listra. Watu wenye walitafuta kumuabudu Paulo, sasa wanamuzunguka na kuanza kumupiga majiwe mupaka anazimia. Kisha kasirani yao kutulia, wanakokotea mwili wa Paulo inje. Juu kisha kumupiga sana, wanawaza kama amekufa.

3. Tutazungumuzia maulizo gani mu hii sura?

3 Ni nini ilifanya mambo iharibike vile? Hii habari ya Barnaba, Paulo, na watu wa Listra wenye walibadilisha mbio mawazo yao inaweza kufundisha nini wahubiri wa leo wa habari njema? Namna gani wazee Wakristo wanaweza kuiga mufano wa Barnaba na Paulo, wanaume waaminifu wenye walivumilia katika utumishi wao, “wakisema bila woga kwa mamlaka ya Yehova”?​—Mdo. 14:3.

“Watu Wengi . . . Wakakuwa Waamini” (Mdo. 14:1-7)

4, 5. Juu ya nini Paulo na Barnaba walienda Ikoniamu, na ni mambo gani yenye ilipitikana kule?

4 Masiku kidogo mbele ya pale, Paulo na Barnaba walifukuzwa mu Antiokia ya Pisidia, muji wa Waroma, kisha Wayahudi wapinzani kuwaletea matatizo. Kuliko kuvunjika moyo juu ya namna wale wakaaji wa Antiokia waliwafukuza, Paulo na Barnaba ‘waliwakungutia mavumbi yenye yalikuwa kwenye miguu yao’ juu hawakupenda kusikiliza. (Mdo. 13:50-52; Mt. 10:14) Paulo na Barnaba wakaondoka kwa amani, wakaenda na kuacha mambo mu mikono ya Mungu. (Mdo. 18:5, 6; 20:26) Wale wamisionere wawili hawakupoteza furaha yao na wakaendelea na safari yao ya kuhubiri. Walisafiri kilometre 150 hivi kusini-mashariki na wakafika eneo tambarare yenye iko kati ya milima ya Taurus na Sultan.

5 Kwanza, Paulo na Barnaba walisimama Ikoniamu. Mu ule muji munayala desturi za Wagiriki na uko kati ya miji ya maana ya jimbo ya Waroma ya Galatia. a Mu ule muji mulikuwa Wayahudi wengi na wageuzwa-imani wenye hawakukuwa Wayahudi. Sawa vile walizoea kufanya, Paulo na Barnaba wakaingia mu sinagogi na wakaanza kuhubiri. (Mdo. 13:5, 14) “Wakasema muzuri sana mupaka watu wengi, Wayahudi na pia Wagiriki wakakuwa waamini.”​—Mdo. 14:1.

6. Juu ya nini Paulo na Barnaba walikuwa walimu wenye kuwa na matokeo ya muzuri, na namna gani tunaweza kuwaiga?

6 Juu ya nini namna ya Paulo na Barnaba ya kusema ilikuwa na matokeo ya muzuri? Paulo alikuwa najua kutumikisha Maandiko kwa hekima. Alitumia kwa ufundi historia, unabii, na Sheria ya Musa ili kuhakikishia watu kama Yesu alikuwa Masiya mwenye aliahidiwa. (Mdo. 13:15-31; 26:22, 23) Namna ya Barnaba ya kuongea ilionyesha kama alihangaikia watu. (Mdo. 4:36, 37; 9:27; 11:23, 24) Wote wawili hawakutegemea uelewaji wao wenyewe, lakini walisema “kwa mamlaka ya Yehova.” Namna gani unaweza kuiga wale wamisionere mu kazi yako ya kuhubiri? Unaweza kuwaiga kwa kufanya hivi: Ujue muzuri Neno ya Mungu. Chagua maandiko yenye inaweza kufurahisha zaidi wasikilizaji wako. Tafuta njia mbalimbali ya kufariji wale wenye unahubiria. Na kila mara mafundisho yako itegemee mamlaka ya Neno ya Yehova, hapana hekima yako mwenyewe.

7. (a) Habari njema inakuwaka na matokeo gani mbalimbali? (b) Kama familia yako inagawanyika kwa sababu uko unatii habari njema, unapaswa kukumbuka nini?

7 Lakini, haiko watu wote mu Ikoniamu njo walifurahia kusikiliza ujumbe wa Paulo na Barnaba. Luka anaeleza hivi: “Wayahudi wenye hawakuamini wakachochea mubaya watu wa mataifa na kuwafanya wapinge ndugu.” Paulo na Barnaba waliona kama ni lazima wabakie juu watetee habari njema. Na “wakatumia wakati murefu wakisema bila woga.” Matokeo ni kwamba, “watu katika muji waligawanyika; wamoja walikuwa upande wa Wayahudi lakini wengine upande wa mitume.” (Mdo. 14:2-4) Leo pia wakati tunahubiri habari njema, watu wanatenda vilevile. Habari njema inaunganisha watu fulani, na inatenganisha wengine. (Mt. 10:34-36) Kama familia yako inagawanyika kwa sababu uko unatii habari njema, kumbuka kama mara mingi watu wanatupinga kwa sababu ya habari za uongo zenye wamesikia. Mwenendo wako wa muzuri unaweza kuonyesha kama mambo yenye watu wanasema juu yetu ni ya uongo, na unaweza hata kusaidia wale wenye wanatupinga wabadilishe mawazo.​—1 Pe. 2:12; 3:1, 2.

8. Juu ya nini Paulo na Barnaba waliondoka Ikoniamu, na mufano wao unatufundisha nini?

8 Kisha wakati fulani, wapinzani wa Ikoniamu wakakamata mupango wa kupiga Paulo na Barnaba majiwe. Wakati wale wamisionere wawili walipata ile habari, wakaamua kuenda kuhubiri mu eneo ingine. (Mdo. 14:5-7) Leo, wahubiri wa habari njema wanatumia pia busara ya vile. Wakati watu wanatupinga kwa maneno, tunasema bila woga. (Flp. 1:7; 1 Pe. 3:13-15) Lakini wakati wanataka kututendea mubaya, tunaepuka kufanya jambo yoyote yenye inaweza kutia maisha yetu ao maisha ya ndugu zetu mu hatari.​—Mez. 22:3.

“Mugeuke . . . kwa Mungu Mwenye Kuishi” (Mdo. 14:8-19)

9, 10. Listra ilikuwa wapi, na tunajua nini juu ya wakaaji wa ile muji?

9 Paulo na Barnaba walienda Listra, eneo yenye ilitawaliwa na Waroma yenye ilikuwa ku kilometre 30 hivi kusini-mangaribi mwa Ikoniamu. Listra ilikuwa na uhusiano wa karibu na Antiokia ya Pisidia. Lakini tofauti na Antiokia ya Pisidia, mu Listra hamukukuwa Wayahudi wengi. Hata kama inawezekana wakaaji wengi wa Listra walizungumuza Kigiriki, luga yao ya kizalikio ilikuwa Kilikaonia. Inawezekana mu Listra hamukukuwa sinagogi. Njo sababu Paulo na Barnaba walianza kuhubiria fasi kwenye kulikuwa watu wengi. Mu Yerusalemu, Petro aliponyesha mwanaume mwenye alizaliwa kilema. Mu Listra, Paulo aliponyesha mwanaume mwenye alizaliwa akiwa kilema wa miguu. (Mdo. 14:8-10) Kwa sababu ya muujiza wenye Petro alifanya, watu wengi walifikia kuwa waamini. (Mdo. 3:1-10) Lakini, ule muujiza wenye Paulo alifanya ulikuwa na matokeo tofauti kabisa.

10 Sawa vile tuliona ku mwanzo wa hii sura, wakati ule mwanaume aliruka na kuanza kutembea, mara moya kikundi ya watu wengi wapagani katika Listra walielewa mubaya ile jambo. Walimuita Barnaba Zeu, mukubwa wa miungu, na Paulo Herme, mwana wa Zeu na musemaji wa miungu. (Ona kisanduku “ Ibada ya Zeu na Herme Katika Listra.”) Hata vile, Barnaba na Paulo waliazimia kusaidia watu kuelewa kama hawakuzungumuza ao kutenda kwa mamlaka ya miungu ya uongo, lakini kwa mamlaka ya Yehova, Mungu mumoja tu wa kweli.​—Mdo. 14:11-14.

“Mugeuke na kuacha mambo haya yenye hayana maana na mukuje kwa Mungu mwenye kuishi, mwenye alifanya mbingu na dunia.”​—Matendo 14:15

11-13. (a) Paulo na Barnaba waliambia nini wakaaji wa Listra? (b) Mambo yenye Paulo na Barnaba walisema inatufundisha nini?

11 Hata kama walikuwa mu hali ya musukosuko, Paulo na Barnaba, walitafuta njia ya muzuri zaidi ya kugusa mioyo ya wasikilizaji wao. Kwa sababu ya ile matukio, Luka aliandika njia ya muzuri ya kuhubiria wapagani habari njema. Ona namna Paulo na Barnaba walijipatanisha na wasikilizaji wao: “Wanaume, sababu gani munafanya mambo haya? Sisi pia ni wanadamu wenye kuwa na uzaifu uleule kama wenu. Na tunawatangazia ninyi habari njema, ili mugeuke na kuacha mambo haya yenye hayana maana na mukuje kwa Mungu mwenye kuishi, mwenye alifanya mbingu na dunia na bahari na vitu vyote vyenye kuwa ndani. Katika vizazi vyenye vilipita aliruhusu mataifa yote waendelee kutembea katika njia zao, hata kama hakukosa kutoa ushahidi juu yake mwenyewe kwa kutenda mema, aliwapatia ninyi mvua kutoka mbinguni na vipindi vya kuzaa matunda, na kuwapatia chakula kwa wingi na kujaza mioyo yenu furaha.”​—Mdo. 14:15-17.

12 Ile maneno yenye kugusa moyo inatufundisha nini? Kwanza, Paulo na Barnaba hawakujiona kuwa wa maana kuliko watu wenye walikuwa wanawasikiliza. Na hawakujionyesha kuwa watu wa pekee. Kuliko kufanya vile, walikubali kwa unyenyekevu kuwa walikuwa na uzaifu kama wale wasikilizaji wao wapagani. Kusema kweli, Paulo na Barnaba walikuwa wamepokea roho takatifu na walikuwa wamewekwa huru kutokana na mafundisho ya uongo. Walipata pia baraka ya kuwa na tumaini ya kutawala pamoya na Kristo. Lakini walijua pia kama ikiwa wakaaji wa Listra wanamutii Kristo, wangeweza pia kupata zile baraka.

13 Tunaonaka namna gani watu wenye tunahubiria? Tunawaonaka kuwa sawasawa na siye? Kama Paulo na Barnaba, wakati tuko nafundisha wengine kweli kumuhusu Mungu, tunaepukaka kutafuta kusifiwa-sifiwa? Charles Taze Russell, mwalimu muzuri, mwenye alikuwa naongoza kazi ya kuhubiri ku mwisho-mwisho wa karne ya 19 na ku mwanzo-mwanzo wa karne ya 20 alituachia mufano muzuri. Aliandika hivi: “Hatujitafutie sifa ao utukufu kwa ajili yetu ao kwa sababu ya maandishi yetu. Wala hatutaki kuitwa Viongozi ao Marabi.” Unyenyekevu wa ndugu Russell unafanana na ule wenye Paulo na Barnaba walikuwa nao. Vilevile, kusudi yetu mu kazi ya kuhubiri haiko kujitafutia sifa, lakini ni kusaidia watu wamugeukie “Mungu mwenye kuishi.”

14-16. Mambo yenye Paulo na Barnaba waliambia wakaaji wa Listra inatufundisha mambo ingine gani?

14 Ona jambo ya pili yenye hii habari inaweza kutufundisha. Paulo na Barnaba walijipatanisha na hali. Tofauti na Wayahudi na wageuzwa-imani wa Ikoniamu, wakaaji wa Listra hawakujua ao pengine walijua tu mambo kidogo juu ya Maandiko ao mambo yenye Mungu alifanyia taifa ya Israeli. Lakini, wale wasikilizaji wa Paulo na Barnaba walijua mambo mingi juu ya kazi ya kulima. Listra ilikuwa na hali ya hewa ya muzuri na udongo wenye ulikomalisha mimea muzuri. Kwa hiyo watu wa Listra wangeona waziwazi sifa za Muumbaji kupitia vipindi vyenye kuzaa matunda. Na wale wamisionere walitumia ile jambo juu ya kugusa mioyo ya wasikilizaji wao.​—Ro. 1:19, 20.

15 Tunaweza pia kujipatanisha na hali? Mulimaji anaweza kupanda aina moya ya mbegu mu shamba mbalimbali, lakini anapaswa kutumia njia tofauti ya kutayarisha udongo mu kila shamba. Aina fulani ya udongo inaweza kuwa teketeke na tayari kwa ajili ya kupanda mbegu. Aina ingine ya udongo inaweza kuwa na lazima ya kutayarishwa zaidi. Vilevile, aina ya mbegu yenye tunapanda ni ileile, ujumbe wa Ufalme wenye kupatikana katika Neno ya Mungu. Lakini, tukiiga Paulo na Barnaba, tutajikaza kutambua hali na imani ya wale wenye tunahubiria. Mambo yenye tunajua kuwahusu itatusaidia tujue namna ya kuwahubiria habari njema.​—Lu. 8:11, 15.

16 Hii habari yenye kuhusu Paulo, Barnaba na wakaaji wa Listra inaweza kutufundisha jambo ingine ya tatu. Hata kama tunajikaza sana, wakati fulani mbegu inaweza kuangukia kwenye miamba ao udongo wenye majiwe-majiwe. (Mt. 13:18-21) Jambo ya vile ikitokea, usivunjike moyo. Sawa vile Paulo alifikiaka kukumbusha wanafunzi Waroma, “kila mumoja wetu [kutia ndani kila mutu mwenye tunahubiria Neno ya Mungu] atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.”​—Ro. 14:12.

“Wakawatia Katika Mikono ya Yehova” (Mdo. 14:20-28)

17. Kisha kutoka Derbe, Paulo na Barnaba walienda wapi na juu ya nini?

17 Kisha Paulo kutupwa inje ya muji wa Listra kwa sababu watu waliwaza kuwa amekufa, mitume walimuzunguka, alisimama, na kisha akapata fasi ya kupitisha usiku mu muji. Siku yenye ilifuata, Paulo na Barnaba walianza safari ya kilometre 100 ya kuenda Derbe. Pima kuwazia vile haikukuwa mwepesi kwa Paulo kufanya ile safari kisha kupigwa majiwe masaa fulani mbele ya pale. Hata vile, yeye na Barnaba walivumilia, na wakati walifika Derbe walifanya “watu wengi kuwa wanafunzi.” Kuliko kupita njia ya mufupi ya kurudia kwao, Antiokia ya Siria, “wakarudia Listra, Ikoniamu, na Antiokia.” Juu ya nini walifanya vile? ili ‘kutia wanafunzi nguvu, kwa kuwatia moyo wabakie katika imani.’ (Mdo. 14:20-22) Bila shaka wale wanaume walituachia mufano muzuri sana! Kuliko kujifikiria, walihangaikia kwanza hali ya muzuri ya kutaniko. Leo waangalizi wenye kusafiri na wamisionere wanaiga mufano wao.

18. Mambo inafanyikaka namna gani ili mutu afikie kuwekwa kuwa muzee?

18 Zaidi ya kutia moyo wanafunzi kupitia maneno na mufano wao, Paulo na Barnaba waliweka “wazee kwa ajili yao katika kila kutaniko.” Hata kama “walitumwa na roho takatifu” mu ile safari ya umisionere, Paulo na Barnaba walisali na kufunga wakati ‘walitia [wanaume wazee] katika mikono ya Yehova.’ (Mdo. 13:1-4; 14:23) Na ni vile mambo inakuwaka leo. Mbele ya kupendekeza ndugu kwa ajili ya madaraka, baraza ya wazee inakuwaka inasali na kuchunguza kama ule ndugu anatimiza mambo yenye Maandiko inaomba. (1 Ti. 3:1-10, 12, 13; Tit. 1:5-9; Yak. 3:17, 18; 1 Pe. 5:2, 3) Hawaangaliake tu miaka yenye amefanya mu tengenezo. Lakini maneno ya ule ndugu, matendo yake, na namna anajulikana njo vinaonyesha ni kwa kadiri gani roho takatifu iko natenda mu maisha yake. Kama anatimiza mambo yenye Maandiko inaomba, ile njo itaonyesha ikiwa anastahili kuwa muchungaji wa kundi. (Gal. 5:22, 23) Mwangalizi wa muzunguko iko na daraka ya kuweka ndugu ku ile madaraka.​—Linganisha na 1 Timoteo 5:22.

19. Wazee wanajua kama watafanya nini, na namna gani wanaiga mufano wa Paulo na Barnaba?

19 Wazee wanajua kama watatoa hesabu kwa Mungu juu ya namna wanatendea kutaniko. (Ebr. 13:17) Kama vile Paulo na Barnaba, wazee wanatuwekea mufano mu kazi ya kuhubiri. Wanatia nguvu Wakristo wenzao kupitia maneno yao. Na kuliko kufikiria faida zao, wanahangaikia kwanza hali ya muzuri ya kutaniko.​—Flp. 2:3, 4.

20. Kusoma kuhusu kazi ya uaminifu ya ndugu zetu, kunatuletea faida gani?

20 Ku mwisho, wakati Paulo na Barnaba walirudia ku makao yao katika Antiokia ya Siria, walieleza “mambo mengi yenye Mungu alikuwa amefanya kupitia wao, na kwamba alikuwa amefungulia mataifa mulango wa kuingia katika imani.” (Mdo. 14:27) Wakati tunasoma kuhusu kazi ya uaminifu ya ndugu zetu na kuona namna Yehova alibariki bidii yao, tutatiwa moyo kuendelea ‘kusema bila woga kwa mamlaka ya Yehova.’

a Ona kisanduku “ Ikoniamu​—Muji wa Wafrigia.”