Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 14

“Tumefikia Uamuzi Mumoja”

“Tumefikia Uamuzi Mumoja”

Namna baraza yenye kuongoza ilikamata uamuzi wa maana na namna ule uamuzi ulifanya mu kutaniko mukuwe umoja

Inategemea Matendo 15:13-35

1, 2. (a) Baraza yenye kuongoza ya mu karne ya kwanza inapaswa kujibia maulizo gani ya maana? (b) Ni mambo gani yenye wako nayo yenye itawasaidia kukamata uamuzi muzuri?

 KILA mutu iko nangoya kwa hamu uamuzi wenye utakamatwa. Mitume wote na wazee wenye kuwa mu ile chumba katika Yerusalemu wanaangaliana. Wanatambua kwamba wako tayari kukamata uamuzi wa maana sana. Tatizo ya kutahiriwa imetokeza maulizo mazito. Wakristo wako chini ya Sheria ya Musa? Kuko tofauti kati ya Wakristo Wayahudi na Wakristo wa mataifa?

2 Wale wanaume wenye kuongoza wamechunguza habari mbalimbali. Wamezungumuzia unabii mbalimbali wa Neno ya Mungu, na wanatoka kusikia ushuhuda wenye nguvu wenye kuonyesha kama Yehova anakubali Wakristo wa mataifa. Kila mutu ametoa mawazo yake juu ya ile jambo. Wamepata habari zote zenye wako nazo lazima ili kukamata uamuzi. Ni wazi kama roho ya Mungu iko naonyesha njia ya kufuata. Wale wanaume watafuata muongozo wa roho ya Mungu?

3. Tutapata faida gani wakati tunachunguza habari yenye kuwa mu kitabu ya Matendo sura ya 15?

3 Inaomba kuwa na imani na uhodari ili kukubali muongozo wa roho ya Mungu mu hii hali. Uamuzi wao unaweza kufanya viongozi wa dini ya Kiyahudi wawachukie hata zaidi. Na watu fulani wenye kuwa mu kutaniko wenye wanapenda watu wa Mungu wafuate Sheria ya Musa, wanaweza kupinga uamuzi wa baraza yenye kuongoza. Baraza yenye kuongoza itafanya nini? Acha tuone. Tutaona pia namna wale wanaume waliachia mufano Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova leo. Sie pia tunapaswa kufuata ile mufano wakati tunapambana na magumu ao wakati tunapaswa kukamata uamuzi wa maana mu maisha yetu ya Kikristo.

“Maneno ya Manabii Yanakubaliana” (Mdo. 15:13-21)

4, 5. Yakobo alitaya maneno gani ya kiunabii yenye kuwa mu Neno ya Mungu?

4 Yakobo, ndugu ya Yesu, akaanza kuzungumuza. a Inawezekana ni yeye njo alikuwa anasimamia ile mukutano. Inaonekana maneno yake ni kifupi ya uamuzi wenye baraza yote ilikamata. Yakobo anaambia hivi watu wote wenye kuwa pale: “Simioni ameeleza kikamili namna Mungu kwa mara ya kwanza alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kati yao watu kwa ajili ya jina lake. Na maneno ya Manabii yanakubaliana na jambo hili.”​—Mdo. 15:14, 15.

5 Inawezekana maneno ya Simioni ao Simoni Petro na ushuhuda wa Paulo na Barnaba ilikumbusha Yakobo maandiko fulani ya maana yenye ilisaidia ndugu waelewe mawazo ya Yehova juu ya ile jambo. (Yoh. 14:26) Kisha kusema kama “maneno ya Manabii yanakubaliana na jambo hili,” Yakobo alitaya maneno yenye kuwa mu Amosi 9:11, 12. Kitabu ya Amosi iko kati ya vitabu vya Maandiko ya Kiebrania vyenye vinazoea kuitwa “Manabii.” (Mt. 22:40; Mdo. 15:16-18) Utatambua kama maneno yenye Yakobo anataya iko tofauti kidogo na yenye inapatikana mu kitabu ya Amosi leo. Inawezekana alitaya maneno ya Septante, tafsiri ya Kigiriki ya Maandiko ya Kiebrania.

6. Namna gani Maandiko ilisaidia ndugu watambue mapenzi ya Mungu?

6 Kupitia Amosi, Yehova alitabiri kama wakati fulani wenye kuya atainua “kibanda cha Daudi,” ni kusema, kizazi ya kifalme yenye kuongoza ku Ufalme wa Kimasiya. (Eze. 21:26, 27) Yehova angetendea tena Waisraeli wa kimwili kwa njia ya pekee? Hapana. Ule unabii unaongeza kama “watu wa mataifa yote” wangekusanywa pamoya na kuwa “watu wenye wanaitwa kwa jina la [Mungu].” Kumbuka kama Petro anatoka tu kutoa ushuhuda kama Mungu “hakufanya tofauti yoyote kati yetu [Wakristo Wayahudi] nao [Wakristo wa Mataifa], lakini alitakasa mioyo yao kwa imani.” (Mdo. 15:9) Ni kusema, mapenzi ya Mungu ni kwamba Wayahudi na Watu wa Mataifa, wote pamoja wariti Ufalme. (Ro. 8:17; Efe. 2:17-19) Hakuna fasi kwenye unabii unaonyesha kama Wakristo wa Mataifa walipaswa kwanza kutahiriwa katika mwili ao kuwa wageuzwa-imani.

7, 8. (a) Yakobo alipendekeza nini? (b) Tunapaswa kuelewa namna gani maneno ya Yakobo?

7 Kwa sababu ya uhakikisho wenye kuwa mu Maandiko ya kiunabii na ushuhuda wenye ametoka kusikia, Yakobo alisema hivi: “Kwa hiyo, uamuzi wangu ni tusisumbue Watu wa Mataifa wenye wanageuka na kuwa upande wa Mungu, lakini kuwaandikia wajiepushe na vitu vyenye vilichafuliwa na sanamu, na uasherati, na vitu vyenye vilinyongwa, na damu. Kwa maana tangu zamani Musa iko na watu wenye wanamuhubiri katika muji mumoja kisha muji mwingine, kwa sababu anasomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila sabato.”​—Mdo. 15:19-21.

8 Wakati Yakobo alisema “kwa hiyo, uamuzi wangu ni,” je, alikuwa nakazia mamlaka yake juu ya ndugu wengine, pengine juu alikuwa musimamizi wa ile mukutano, na kuamua yeye mwenyewe namna mambo ilipaswa kuwa? Hapana kabisa! Neno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “uamuzi wangu ni” inaweza pia kumaanisha “Ninaona kama” ao “Mawazo yangu ni.” Yakobo hakukuwa hata kidogo anakamata uamuzi kwa ajili ya baraza yote. Alikuwa tu anatoa mawazo yake kuhusu mambo yenye ilipaswa kufanywa kisha kusikiliza ushuhuda wenye ulikuwa umetolewa, na mambo yenye Maandiko inasema kuhusu ile jambo.

9. Pendekezo ya Yakobo ilileta faida gani?

9 Pendekezo ya Yakobo ilikuwa ya muzuri? Bila shaka ilikuwa ya muzuri, juu mitume na wazee waliikubali. Ile ilileta faida gani? Faida ya kwanza ni hii: ule uamuzi ‘haungesumbua’ ao kufanya mambo ikuwe nguvu kwa Watu wa Mataifa kwa kuwalazimisha washike Sheria ya Musa. (Mdo. 15:19) Na faida ingine, ule uamuzi ungeheshimia zamiri ya Wakristo Wayahudi wenye kwa miaka mingi walisikiliza “Musa . . . anasomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila sabato.” b (Mdo. 15:21) Ule uamuzi ungesaidia Wakristo wa Mataifa na Wakristo Wayahudi wapendane hata zaidi. Na zaidi ya yote, ule uamuzi ungemufurahisha Yehova kwa sababu ulipatana na mapenzi yake. Bila shaka ile ni namna ya muzuri ya kushugulikia tatizo yenye ingevuruga amani na umoja wa kutaniko! Na ni mufano muzuri kwa kutaniko ya Kikristo leo!

Albert Schroeder iko natoa hotuba ku mukusanyiko wa kimataifa wa 1998

10. Namna gani Baraza Yenye Kuongoza leo inaiga mufano wa baraza yenye kuongoza ya mu karne ya kwanza?

10 Sawa vile tuliona mu sura yenye ilitangulia, Baraza Yenye Kuongoza leo inafuata mufano wa baraza yenye kuongoza ya wakati wa mitume. Mu mambo yote inatafutaka muongozo wa Yehova, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, na Yesu Kristo, Kichwa ya kutaniko. c (1 Ko. 11:3) Wanafanyaka vile namna gani? Albert D. Schroeder, mwenye alitumikia mu Baraza Yenye Kuongoza kuanzia mwaka wa 1974 mupaka Mwezi wa 3, 2006, wakati maisha yake ya ku dunia ilifikia mwisho, alisema hivi: “Ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wanakutanaka Siku ya Tatu, wanaanzaka mukutano na sala ili kumuomba Yehova muongozo wa roho takatifu. Wanafanyaka yao yote ili kuhakikisha kama kila jambo na kila uamuzi wenye wanakamata unapatana na Neno ya Mungu, Biblia.” Vilevile, Milton G. Henschel, mwenye alitumikia miaka mingi mu Baraza Yenye Kuongoza na mwenye maisha yake hapa ku dunia ilifikia mwisho mu Mwezi wa 3, 2003, aliulizaka wanafunzi wa darasa ya 101 ya Gileadi ulizo ya maana sana. Aliwaulizaka hivi: “Kuko tengenezo ingine hapa ku dunia yenye Baraza yake Yenye Kuongoza inachunguzaka Neno ya Mungu Biblia mbele ya kukamata maamuzi ya maana?” Jibu iko wazi.

“Kutuma Wanaume Wenye Walichaguliwa” (Mdo. 15:22-29)

11. Uamuzi wa baraza yenye kuongoza ulifikia makutaniko namna gani?

11 Ndugu wa baraza yenye kuongoza katika Yerusalemu wamekubaliana na wamekamata uamuzi kuhusu tatizo ya kutahiriwa. Ili ndugu mu makutaniko watende kwa umoja, wanapaswa kujulishwa ile uamuzi mu njia yenye kuwa wazi na yenye kutia moyo. Baraza yenye kuongoza ingefanya vile namna gani? Habari inaendelea hivi: “Mitume na wazee, pamoja na kutaniko lote, wakaamua kutuma wanaume wenye walichaguliwa kutoka kati yao waende Antiokia, pamoja na Paulo na Barnaba; walituma Yuda mwenye aliitwa Barsaba pamoja na Sila, wanaume wenye walikuwa wanaongoza kati ya ndugu.” Zaidi ya ile, waliandika barua na kuipatia wale wanaume ili isomwe mu makutaniko yote yenye kuwa Antiokia, Siria, na Kilikia.​—Mdo. 15:22-26.

12, 13. Zungumuzia faida ya kutuma (a) Yuda na Sila (b) barua kutoka kwa baraza yenye kuongoza.

12 Yuda na Sila walikuwa “wanaongoza kati ya ndugu.” Kwa hiyo, walistahili kuwa wajumbe wa baraza yenye kuongoza. Wanaume ine wenye walitumwa wangeonyesha wazi kama ujumbe wenye wanaleta haiko tu jibu yenye kuhusu kutahiriwa, lakini ni muongozo mupya kutoka kwa baraza yenye kuongoza. Wale wanaume wenye “walichaguliwa” wangesaidia kukuwe umoja kati ya Wakristo wa Mataifa wenye kuwa mu makutaniko na Wakristo Wayahudi wenye kuwa Yerusalemu. Kutuma wale wanaume ilikuwa uamuzi wenye hekima na wenye upendo! Bila shaka ile ilisaidia kuendeleza umoja na amani kati ya watu wa Mungu.

13 Ile barua ilitolea Wakristo wa Mataifa muongozo kuhusu kutahiriwa, lakini pia kuhusu mambo yenye walipaswa kufanya ili Yehova awakubali na awabariki. Sehemu ya maana sana ya ile barua ilisema hivi: “Roho takatifu na sisi wenyewe tumeona ni muzuri tusiwaongezee ninyi muzigo zaidi, isipokuwa mambo haya ya lazima: kuendelea kujiepusha na vitu vyenye vilitolewa zabihu kwa sanamu, na damu, na vitu vyenye vilinyongwa, na uasherati. Kama munajiepusha kwa uangalifu na mambo haya, mambo yatakuwa muzuri kwenu. Afya njema kwenu!”​—Mdo. 15:28, 29.

14. Nini njo inasaidia watu wa Mungu waendelee kuwa na umoja leo mu dunia yenye kugawanyika?

14 Leo, Mashahidi wa Yehova wako na umoja wa kweli. Wanaamini mambo ileile na wanafanya kazi ileile hata kama wako zaidi ya 8000000 mu makutaniko zaidi ya 100000 mu dunia yote. Namna gani ile inawezekana leo mu hii dunia yenye kuwa na muvurugo na yenye watu hawana umoja? Jambo ya kwanza yenye inawasaidia wakuwe na umoja ni juu wanapata muongozo wenye kuwa wazi kutoka kwa Kristo, Kichwa ya kutaniko, kupitia “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” ni kusema, Baraza Yenye Kuongoza. (Mt. 24:45-47) Pia, tunakuwaka na umoja kwa sababu ndugu na dada wa mu dunia yote wanakuwaka tayari kufuata muongozo wa Baraza Yenye Kuongoza.

“Wakafurahi Sana Juu ya Kitia-Moyo Hicho” (Mdo. 15:30-35)

15, 16. Makutaniko ilitenda namna gani kisha kupokea muongozo wa baraza yenye kuongoza, na juu ya nini ilitenda vile?

15 Habari yenye kuwa mu kitabu ya Matendo inaendelea kufasiria kama wakati wale ndugu wenye walitumwa kutoka Yerusalemu walifika Antiokia, ‘walikusanya kikundi chote pamoja na kuwapatia barua hiyo.’ Ndugu wa Antiokia walitenda namna gani kisha kupata muongozo wa baraza yenye kuongoza? “Kisha kuisoma [ile barua], wakafurahi sana juu ya kitia-moyo hicho.” (Mdo. 15:30, 31) Zaidi ya ile, Yuda na Sila “wakatia ndugu moyo kwa hotuba nyingi na wakawatia nguvu.” Ni mu ile njia njo wale wanaume wawili walikuwa “manabii,” sawa vile Barnaba, Paulo, na wengine waliitwa manabii, neno yenye kuzungumuzia wale wenye kutangaza ao kujulisha wengine mapenzi ya Mungu.​—Mdo. 13:1; 15:32; Kut. 7:1, 2.

16 Bila shaka Yehova alibariki ule mupango wa baraza yenye kuongoza na ile ilitia moyo makutaniko yote. Juu ya nini makutaniko ilitiwa moyo? Ni kwa sababu muongozo wa baraza yenye kuongoza ulikuwa wazi na ulitolewa kwa wakati wenye kufaa. Zaidi ya ile ulitegemea Neno ya Mungu na muongozo wa roho takatifu. Tena, ule uamuzi ulitangazwa ku makutaniko kwa njia ya upendo na huruma.

17. Namna gani waangalizi wa muzunguko leo wanafuata mufano wa Paulo, Barnaba, Yuda, na Sila?

17 Leo, Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova inafuata ile mufano kwa kutolea ndugu wa mu dunia yote muongozo kwa wakati wenye kufaa. Wakati wanakamata maamuzi, wanaitangazia makutaniko mu njia yenye kuwa wazi na yenye kueleweka muzuri. Wakati fulani wanatumia waangalizi wa muzunguko ili kupatia makutaniko maagizo. Wakati wale ndugu wenye kujitoa wanasafiri mu makutaniko mbalimbali, wanatolea ndugu muongozo wenye kuwa wazi na kuwatia moyo. Sawa vile Paulo na Barnaba, wale ndugu wanapitisha wakati mingi mu mahubiri, “wakifundisha na kutangaza habari njema ya neno la Yehova pamoja na wengine wengi.” (Mdo. 15:35) Sawa Yuda na Sila, wanatia ‘ndugu moyo kwa hotuba nyingi’ na wanawatia nguvu.

18. Watu wa Mungu wanapaswa kufanya nini ili kuendelea kupata baraka ya Yehova?

18 Tuseme nini juu ya makutaniko? Ni nini inasaidia makutaniko ya mu dunia yote iendelee kuwa na amani na umoja mu hii dunia yenye kugawanyika? Kumbuka kama ni mutume Yakobo njo alifikiaka kuandika hivi: “Hekima yenye inatoka juu kwanza kabisa ni safi, kisha yenye kufanya amani, yenye usawaziko, tayari kutii . . . Zaidi ya hayo, tunda la haki linapandwa katika hali zenye amani kwa ajili ya wale wenye kufanya amani.” (Yak. 3:17, 18) Hatujue kama Yakobo alikuwa anafikiria ile mukutano yenye ilifanyikaka Yerusalemu wakati alikuwa anaandika ile maneno. Lakini wakati tunachunguza habari yenye kuwa mu sura ya 15 ya kitabu ya Matendo, tunaelewa kama Yehova anaweza tu kutubariki ikiwa tuko na umoja na kama tunatumika pamoja.

19, 20. (a) Nini ilionyesha kama amani na umoja ilikuwa mu kutaniko ya Antiokia? (b) Paulo na Barnaba wangefanya sasa nini?

19 Amani na umoja yenye ilikuwa sasa mu kutaniko ya Antiokia ilionekana wazi. Kuliko kubishana na ndugu wenye walitoka Yerusalemu, ndugu wa Antiokia walifurahia ziara ya Yuda na Sila. Habari inaendelea hivi: “Kisha kupitisha wakati fulani kule, ndugu hao wakawaacha warudie kwa amani kwa wale wenye walikuwa wamewatuma,” ni kusema, walirudia Yerusalemu. d (Mdo. 15:33) Tunaweza kuwa hakika kama ndugu wa Yerusalemu walifurahi pia wakati wale wanaume wawili waliwapatia ripoti ya safari yao. Kwa fazili zenye hazistahiliwe za Yehova, mugao wao ulipita muzuri!

20 Paulo na Barnaba, wenye walibakia Antiokia, wangekazia sasa kazi ya kuhubiri na kuwekea wengine mufano. Ni vile waangalizi wa muzunguko wanafanyaka leo wakati wanatembelea makutaniko. (Mdo. 13:2, 3) Wale ndugu ni baraka kabisa kutoka kwa Yehova. Sasa namna gani Yehova aliendelea kutumikisha na kubariki wale waeneza-injili wawili wenye bidii? Tutaona jibu ya ile ulizo mu sura yenye kufuata.

Wakristo leo wanafaidika na chakula ya kiroho kutoka kwa Baraza Yenye Kuongoza na wajumbe wake

a Ona kisanduku “ Yakobo​—‘Ndugu ya Bwana.’

b Kwa hekima Yakobo alizungumuzia maandishi ya Musa. Ile maandishi haikukuwa tu Sheria ya Musa, lakini ilitia ndani habari zenye kuonyesha mapenzi ya Mungu ilikuwa nini kwa ajili ya wanadamu wote, hata mbele atoe Sheria ya Musa. Kwa mufano, mu kitabu ya Mwanzo tunaona mawazo ya Mungu juu ya damu, uzinifu, na kuabudu sanamu. (Mwa. 9:3, 4; 20:2-9; 35:2, 4) Kwa hiyo Yehova alitoa kanuni zenye wanadamu wote wanapaswa kufuata ikuwe ni Wayahudi ao Watu wa Mataifa.

d Mu mustari wa 34, tafsiri fulani za Biblia zinaongeza maneno yenye kuonyesha kama Sila aliamua kubakia Antiokia. (King James Version) Lakini, inaonekana ile maneno iliongezwa kisha.