Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Barua Kutoka kwa Baraza Yenye Kuongoza

Barua Kutoka kwa Baraza Yenye Kuongoza

Muhubiri Mupendwa wa Ufalme:

Ujiwazie kuwa mumoja kati ya wale mitume wenye kusimama pale ku Mulima wa Mizeituni. Yesu anatokea mbele yako. Mbele tu apande mbinguni, anasema: “Mutapokea nguvu wakati roho takatifu itakuja juu yenu, na mutakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Utatenda namna gani?

Pengine utaona sawa vile anawaachia kazi kubwa sana. Unaweza kujiuliza, ‘Namna gani, siye hesabu kidogo ya wanafunzi, tutatoa ushahidi “mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia”’? Pengine unakumbuka onyo yenye Yesu alitoa usiku mbele akufe: “Mutumwa haiko mukubwa kuliko bwana wake. Kama wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia; kama wameshika neno langu, watashika lenu pia. Lakini watawatendea ninyi mambo yote haya kwa sababu ya jina langu, kwa kuwa hawajue Ule mwenye alinituma.” (Yoh. 15:20, 21) Ile maneno inaweza kufanya ujiulize hivi: ‘Namna gani ninaweza kutoa ushahidi kamili mu hii upinzani na mateso yote?’

Leo pia tuko najiuliza maulizo ya vile. Na siye Mashahidi wa Yehova, kazi yetu inaomba kutoa ushahidi kamili “mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia,” kwa “watu wa mataifa yote.” (Mt. 28:19, 20) Hii kazi inaweza kutimizwa namna gani, zaidi sana katika upinzani wenye ulitabiriwa?

Kitabu ya Matendo ya Mitume inatutolea habari yenye kutuchochea kabisa ya namna mitume na ndugu na dada zao wa mu karne ya kwanza waliweza kutimiza mugao wao kwa musaada wa Yehova. Kusudi ya hii kitabu yenye uko unasoma ni kukusaidia uchunguze zile habari na zikuchochee kabisa kutenda. Utashangala kuona mambo yenye kufanana kati ya watumishi wa Mungu wa wakati wa mitume na watu wa Mungu leo. Utaona kama ile mambo haitie ndani tu kazi yenye tuko nafanya lakini pia namna tunapangwa juu ya kufanya ile kazi. Bila shaka, ile mambo yenye kufanana itafanya imani yako ikuwe nguvu, na itakusaidia ukuwe hakika kabisa kama ni Yehova Mungu njo iko naongoza hii sehemu ya ku dunia ya tengenezo yake.

Tunaendelea kusali na kuwa hakika kama, kuchunguza kitabu ya Matendo kutakusadikisha kabisa kama Yehova atakusaidia, na kama nguvu ya roho takatifu yake itakutegemeza. Tunakutia moyo uendelee “kutoa ushahidi kamili” juu ya Ufalme wa Mungu na kusaidia wengine wafikie kutembea mu njia yenye kuongoza kwenye wokovu.​—Mdo. 28:23; 1 Ti. 4:16.

Ndugu zako,

Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova