Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO YA 1

Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?

Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?

Wakati ulikuwaka mutoto kidogo, kuko siku uliulizaka wazazi wako kama watoto wanatokaka wapi? Kama uliwaulizaka, walikujibiaka nini? Pengine wazazi wako hawakukujibiaka kitu juu ulikuwa ungali mutoto na juu ya namna yao ya kuwa. Ao pengine walisikiaka haya na wakakujibia tu mbio-mbio. Ao tena, pengine walikuambiaka hadisi fulani ya kujitungia na wakati ulikomala ulifikia kujua kama ilikuwa ya uongo. Ili kumutayarisha mutoto kwa ajili ya maisha ya bukubwa na ya ndoa, inaomba kumufundisha vile mutoto anafikiaka kuzaliwa.

Sawa vile tu wazazi wengi wanasikiaka haya ya kueleza vile mutoto anafikiaka kuzaliwa, wanasayansi wengi wanakuwaka wanasita kuzungumuzia hii ulizo ya maana: Vitu vyenye uzima vilitoka wapi? Kama mutu anapata jibu ya muzuri kwa ile ulizo, ile inaweza kumusaidia akuwe na mawazo ya muzuri juu ya uzima. Sasa, vitu vyenye vilianza namna gani?

Chembe ya liyai ya mwanamuke yenye ilishaungana na mbegu ya uzazi ya mwanaume. Hii picha imenenepeshwa mara 800 hivi

Wanasayansi wengi wanasema nini? Watu wengi wenye kuamini mageuzi wanasema kama kitu ya kwanza yenye uzima ilianza mamiliare ya miaka yenye imepita pembeni ya kiziwa fulani ya maji ao ndani kabisa ya bahari. Wanawaza kama ni fasi sawa ile njo molekile za kidogo-kidogo zilijikusanyaka pamoja na kufanyiza vitu vyenye kuwa sawa pofu, kisha vile vitu vikafanyiza molekile za ajabu sana, na kuanza kujigawanya-gawanya. Wanaamini kama vitu vyote vyenye uzima vyenye kuwa ku dunia vilijitokeza kutokana na chembe moja ao zaidi.

Lakini wanasayansi wengine wenye kuheshimiwa na wenye wanaamini mageuzi hawakubaliane na ile mawazo. Wanasema kama chembe za kwanza-kwanza, ao tuseme sehemu kubwa zenye kufanyiza zile chembe zilitokaka mu anga. Juu ya nini wanasema vile? Juu, hata kama wanasayansi wamejikaza sana ili kuonyesha kama kitu yenye uzima inaweza kutokana na molekile zenye hazina uzima, wameshindwa kufanya vile. Mu mwaka wa 2008, Alexandre Meinesz, mwalimu wa biolojia ku masomo ya juu, alizungumuzia ile jambo. Alisema kama kwa miaka zaidi ya 50 yenye imepita, “hakuna ushuhuda wenye kutegemeka wenye unaonyesha kama vitu vyenye uzima vilijitokeza kutokana na molekile fulani, na hakuna maendeleo mu mambo ya sayansi yenye inaonyesha vile.”1

Ushuhuda unaonyesha nini? Vitabu mingi vilishakafasiria kwenye watoto wanatokaka, na hakuna mutu mwenye anaweza kupinga ile mafasirio. Kitu yenye uzima inatokanaka tu na kitu ingine yenye uzima. Lakini, tukirudia nyuma miaka mingi sana yenye imepita, inawezekana ile sheria ya musingi ilivunjwa? Kweli kabisa vitu vyenye uzima vilijitokeza kutokana na molekile zenye hazina uzima? Ni kwa kadiri gani inawezekana ile jambo itokee?

Watu wenye kufanya uchunguzi wamevumbula kama, kusudi chembe iendelee kuishi, inaomba aina tatu hivi za molekile za ajabu zifanye kazi pamoja: ADN (acide désoxyribonucléique), ARN (acide ribonucléique) na proteine mbalimbali. Leo, ni wanasayansi kidogo tu njo wanaweza kusema kama chembe yenye uzima ilijitokeza kutokana na muchanganyiko wa molekile zenye hazina uzima. Lakini, kuko uwezekano gani ARN ao proteine ijitokeze? *

Stanley Miller, mu mwaka wa 1953

Jambo fulani yenye ilifanywa kwa mara ya kwanza mu 1953 njo ilifanya wanasayansi wengi wawaze kama vitu vyenye uzima vilijitokeza. Mu ile mwaka, Stanley Miller aliweza kutengeneza aside-amine, ni kusema, molekile za musingi zenye zinafanyiza proteine. Alifanya vile kwa kupitisha umeme (courant) mu muchanganyiko wa gaze wenye uliwaziwa kama ulifananisha anga ya kwanza-kwanza ya dunia. Kuanzia ile wakati, aside-amine zimepatikana pia katika meteorite (vitu vyenye kuwa sawa majiwe vyenye vinaangukaka ku dunia kutoka mu anga). Mambo yenye walivumbula inaonyesha kama molekile za musingi zenye kufanyiza vitu vyenye uzima zinaweza kujitokeza?

Robert Shapiro, mwenye alikuwaka mwalimu wa chimie ku masomo ya juu ya New York, anasema hivi: “Watu fulani wamewaza kama molekile zote za musingi zenye kufanyiza vitu vyenye uzima zinaweza kutengenezwa kwa vyepesi kwa kufanya mambo yenye Miller alifanyaka, na kama zinapatikana mu meteorite. Lakini, ile haiko kweli.”2 *

Fikiria molekile ya ARN. Inafanyizwa na molekile za kidogo-kidogo zenye kuitwa nikleotide. Nikleotide ni aina ya molekile yenye kuwa tofauti na aside-amine na ni ya ajabu zaidi kidogo kuliko aside-amine. Shapiro anasema kama hakuna aina yoyote ya nikleotide yenye imetengenezwa kwa kutumia ufundi wa Miller, ao yenye imepatikana mu meteorite.3 Anasema tena kama uwezekano wa molekile mbalimbali kujikusanya pamoja na kufanyiza molekile moja ya ARN yenye inaweza kujigawanya-gawanya “ni mudogo sana kiasi ya kwamba, ni nguvu kuwazia kama ile jambo inaweza kutokea hata mara moja fasi fulani ku dunia.”4

ARN (1) ni ya lazima ili kutengeneza proteine (2), proteine nazo ni za lazima ili kutengeneza ARN. Ingewezekana namna gani zile molekile zijitokeze? Ribozome (3) zitazungumuziwa mu ulizo ya 2.

Tuseme nini juu ya molekile za proteine? Zinaweza kufanyizwa na aside-amine 50 hivi ao hata maelfu ya aside-amine zenye zinaunganishwa pamoja mu mupangilio wa hali ya juu sana. Kwa kukadiria, mu chembe moja, proteine moja iko na aside-amine 200. Zaidi ya ile, mu chembe moja, muko maelfu ya aina mbalimbali za proteine. Uwezekano wa proteine moja yenye iko na aside-amine 100 tu kujitokeza, umekadiriwa kuwa mara moja tu hivi kisha ile jambo kujaribu kufanyika mara milioni miliare.

Inaomba mutu mwenye akili sana ili kutengeneza molekile za ajabu sana mu laboratware. Halafu molekile za ajabu zaidi zenye kuwa mu chembe, unawaza zilijitokezaka?

Hubert Yockey, muchunguzi mwenye anaamini mageuzi, anapeleka mawazo mbali, kwa kusema hivi: “Kuhusu namna vitu vyenye uzima vilianzaka, haiwezekane proteine njo zikuwe zenye zilitokeaka kwanza.”5 Proteine haziwezi kutengenezwa kama hakuna ARN, lakini ARN nayo haiwezi kutengenezwa kama hakuna proteine. Hata kama kuko uwezekano mudogo sana, tuseme basi kama proteine na ARN zilijitokeza fasi ileile na wakati ileile. Kama ni vile, ingewezekana namna gani zijiunge pamoja na kutokeza vitu vyenye uzima vyenye viko na uwezo wa kuzalana na kuendelea kuishi? Carol Cleland *, mushiriki wa NASA (National Aeronautics and Space Administration’s Astrobiology Institute) anasema hivi: “Uwezekano wa mambo kufanyika vile yenyewe tu (ndani ya muchanganyiko wenye haupangwe muzuri wa proteine na ARN) ni mudogo sana, tena sana.” Anasema tena hivi: “Hata vile, inaonekana watu wengi wenye kufanya uchunguzi wanawaza kama, ikiwa wanafikia kuelewa namna proteine na ARN zinajitengenezaka zenyewe kwa njia ya asili, haitakuwa nguvu kuelewa namna proteine na ARN zinajiungaka pamoja.” Kuhusu mawazo yenye watu wengi wako nayo leo, yenye kuonyesha kama molekile zenye kufanyiza vitu vyenye uzima zilijitokezaka, Cleland, anasema hivi: “Hakuna mawazo yenye inafasiria muzuri-muzuri namna ile jambo ilifanyikaka.”6

Kama inaomba mutu mwenye akili ili kutengeneza robo yenye haina uzima na kutia ndani maagizo ya kuisadia ifanye kazi, tuseme nini juu ya kutengeneza chembe yenye uzima ao hata mwanadamu?

Kujua ile mambo kuko na faida gani? Fikiria tatizo yenye watu wenye kufanya uchunguzi wenye wanaamini kama vitu vyenye uzima ulijitokeza wanakutanaka nayo. Wamepata mu meteorite aside-amine fulani zenye zinapatikana pia mu chembe fulani zenye uzima. Kwa kutumia ufundi wa kisayansi wa hali ya juu, wametengeneza molekile za ajabu zaidi mu laboratware zao. Wanatumaini kama kuko siku watafikia kutengeneza sehemu zote zenye zinaombwa ili kufanyiza chembe moja. Tunaweza kuwalinganisha na fundi mwenye anatumia vitu vya asili ili kutengeneza chuma, plastike, silikone, na singa. Kisha, anatumia vile vitu ili kutengeneza robo. Kisha tena, anatia mu ile robo maagizo juu nayo itengeneze robo zingine za kuifanana. Wakati anafanya vile, anaonyesha nini? Kwa kweli, anaonyesha kama ni mutu mwenye akili tu njo anaweza kutengeneza mashine ya ajabu sana.

Vilevile, kama siku fulani wanasayansi wataweza kutengeneza chembe, watakuwa wametimiza jambo ya ajabu sana. Lakini, watawezaka kabisa kuonyesha kama chembe inaweza kujitokeza? Kama kuko siku wataweza kutengeneza chembe, bila shaka watakuwa wanaonyesha kama chembe haiwezi kujitokeza?

Unawaza nini? Leo, uchunguzi wote wa wanasayansi unaonyesha kama kitu yenye uzima inatokanaka tu na kitu ingine yenye uzima. Inaomba kuwa na imani sana ili kuitika kama chembe yenye uzima ilijitokezaka kutokana na molekile zenye hazina uzima.

Kufuatana na mambo yote yenye tumeona, uko na sababu kabisa ya kuitika kama chembe yenye uzima ilijitokezaka? Mbele ya kujibia ile ulizo, tuchunguze namna chembe zimefanyizwa. Ile itakusaidia uamue ikiwa mawazo ya wanasayansi fulani kuhusu namna vitu vyenye uzima vilianzaka ni ya kweli, ao inafanana habari za kujitungia zenye wazazi fulani wanaelezeaka watoto wao juu ya kuwafasiria vile watoto wanafikiaka kuzaliwa.

^ Uwezekano wa ADN kujitokeza utazungumuziwa mu ulizo ya 3, yenye kichwa “Maagizo Yote Yenye Kuwa mu ADN Ilitoka Wapi?

^ Shapiro haamini kama vitu vyenye uzima viliumbwa. Anaamini kama vilijitokeza mu njia fulani yenye haiyajulikana. Mu mwaka wa 2009, wanasayansi ku masomo ya juu ya Manchester, Uingereza, walisema kama waliweza kutengeneza nikleotide mu laboratware yao. Lakini, Shapiro anasema kama njia yenye walitumia “ili kutengeneza zile nikleotide haiheshimie kanuni zenye zinakubalika ili kutengeneza ARN.”

^ Cleland haamini habari ya Biblia juu ya uumbaji. Anaamini kama vitu vyenye uzima vilijitokezaka mu namna yenye bado haiyaeleweka muzuri.