Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 2

Mungu wa Kweli ni Nani?

Mungu wa Kweli ni Nani?

Kuna Mungu mmoja tu wa kweli, na jina lake ni Yehova. (Zaburi 83:18) Yeye ni Roho; hatuwezi kumwona. Anatupenda, naye anataka tumpende. Anataka tuwapende watu wengine pia. (Mathayo 22:35-40) Yeye ndiye Aliye Juu Zaidi, Muumba wa vitu vyote.

Kiumbe wa kwanza aliyeumbwa na Mungu alikuwa mtu wa roho mwenye nguvu ambaye baadaye aliitwa Yesu Kristo. Yehova aliwaumba malaika pia.

Yehova aliumba kila kitu mbinguni . . . na duniani. Ufunuo 4:11

Yehova Mungu aliumba nyota na pia dunia na kila kitu kilicho duniani.​—Mwanzo 1:1.

Alimuumba mwanamume wa kwanza, Adamu, kutoka katika mavumbi ya ardhi.—Mwanzo 2:7.