Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 2

Mungu wa Kweli Ni Nani?

Mungu wa Kweli Ni Nani?

Kuko Mungu mumoja tu wa kweli na jina lake ni Yehova. (Zaburi 83:18) Yeye ni Roho; hatuwezi kumuona. Anatupenda na anataka sisi pia tumupende. Anataka pia tupende watu wengine. (Matayo 22:35-40) Iko Mweza-Yote, Muumbaji wa vitu vyote.

Mbele ya kuumba vitu vingine vyote, Mungu aliumba kwanza malaika mumoja mwenye nguvu, mwenye alifikia kuitwa Yesu Kristo. Yehova aliumba pia malaika wengine.

Yehova aliumba kila kitu chenye kuwa mbinguni . . . na kila kitu chenye kuwa ku dunia. Ufunuo 4:11

Yehova Mungu aliumba nyota, dunia, na kila kitu chenye kuwa ku dunia.​—Mwanzo 1:1.

Alitumia mavumbi ya udongo ili kumufanya Adamu, mwanaume wa kwanza.​—Mwanzo 2:7.