Watu wengi katika siku za Noa walitenda mabaya. Mwanzo 6:5
Adamu na Hawa walipata watoto, na watu wakawa wengi duniani. Baada ya muda, malaika fulani walijiunga na Shetani katika uasi wake.
Wakaja duniani na wakajifanyia miili ya kibinadamu ili waweze kuoa wanawake. Wanawake hao wakazaa wana wenye kutisha na wenye nguvu waliokuwa na uwezo unaopita wa wanadamu.
Ulimwengu ukajaa watu waliofanya mambo mabaya. Biblia inasema: “Uovu wa mwanadamu ulikuwa mkubwa duniani na kwamba kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake ulikuwa mbaya tu wakati wote.”