Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 6

Tunajifunza Nini Kutokana na Gharika Kubwa?

Tunajifunza Nini Kutokana na Gharika Kubwa?

Mungu aliwaharibu waovu lakini akamwokoa Noa na familia yake. Mwanzo 7:11, 12, 23

Mvua ilinyesha kwa siku 40 mchana na usiku, nayo maji yakaifunika dunia yote. Watu wote waovu wakafa.

Malaika waasi waliiacha miili yao ya kibinadamu nao wakawa roho waovu.

Watu waliokuwa ndani ya safina waliokoka. Ingawa mwishowe Noa na familia yake walikufa, Mungu atawafufua ili waishi milele.

Mungu atawaharibu waovu tena na kuwaokoa watu wema. Mathayo 24:37-39

Shetani na roho waovu wanaendelea kuwapotosha watu.

Leo, kama ilivyokuwa katika siku za Noa, watu wengi wanakataa mwongozo wenye upendo wa Yehova. Hivi karibuni, Yehova atawaharibu watu wote waovu.​—2 Petro 2:5, 6.

Kuna watu walio kama Noa. Wanamsikiliza Mungu na kufanya mambo anayosema; watu hao ni Mashahidi wa Yehova.