Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 6

Garika Kubwa Inatufundisha Nini?

Garika Kubwa Inatufundisha Nini?

Mungu aliua watu wabaya lakini aliokoa Noa na watu wa familia yake. Mwanzo 7:11, 12, 23

Mvua ilinyesha siku 40 muchana na usiku, na maji ilifunika dunia yote. Watu wabaya wote walikufa.

Wale malaika wenye walimupinga Mungu waliacha miili ya watu na wakakuwa pepo wachafu.

Watu wenye walikuwa mu safina waliokoka. Hata kama Noa na watu wa familia yake walifikia kufa, Mungu atawafufua na watakuwa na tumaini la kuishi milele.

Mungu ataua tena watu wabaya na kuokoa watu wazuri. Matayo 24:37-39

Shetani na pepo wake wachafu wanaendelea kudanganya watu.

Kama wakati wa Noa, leo watu wengi hawamutii ao kumusikia Yehova. Karibuni Yehova ataua watu wote wabaya.​—2 Petro 2:5, 6.

Watu fulani wako kama Noa. Wanamusikiliza Mungu na wanafanya mambo yenye anasema; wale watu ni Mashahidi wa Yehova.