SEHEMU YA 8

Kifo cha Yesu Kinamaanisha Nini Kwako?

Kifo cha Yesu Kinamaanisha Nini Kwako?

Yesu alikufa ili tuweze kuishi. Yohana 3:16

Siku tatu baada ya Yesu kufa, wanawake fulani walienda kwenye kaburi lake na kulipata likiwa tupu. Yehova alikuwa amemfufua Yesu.

Baadaye, Yesu aliwatokea mitume wake.

Ndiyo, Yehova alimfufua Yesu akiwa kiumbe wa roho mwenye nguvu, na asiyeweza kufa. Wanafunzi wa Yesu walimwona akipaa kwenda mbinguni.

Mungu alimfufua Yesu na kumfanya awe Mfalme wa Ufalme wa Mungu. Danieli 7:13, 14

Yesu alitoa uhai wake ili kulipa fidia kwa ajili ya wanadamu. (Mathayo 20:28) Hivyo, kupitia fidia hiyo Mungu anafanya iwezekane kwetu kuishi milele.

Yehova alimchagua Yesu kuwa Mfalme juu ya dunia. Atatawala pamoja na watu waaminifu 144,000, ambao wanafufuliwa kutoka duniani na kwenda kuishi mbinguni. Yesu na hao 144,000 wanafanyiza serikali ya kimbingu yenye uadilifu, yaani, Ufalme wa Mungu.—Ufunuo 14:1-3.

Ufalme wa Mungu utaifanya dunia kuwa paradiso. Hakutakuwa tena na vita, uhalifu, umaskini, na njaa. Watu watakuwa na furaha kwelikweli.—Zaburi 145:16.