SEHEMU YA 14
Utafanya Nini ili Kuonyesha Kama Uko Mushikamanifu kwa Yehova?
Ujitie ngambo ya Mungu. 1 Petro 5:6-9
Uepuke desturi zote zenye hazipatane na Biblia. Ili ufanye vile, inaomba usiogope watu.
Usijiingize mu mambo ya politike; ile mambo haimuunge Yehova mukono na Ufalme wake.
Matayo 7:24, 25
Ukamate uamuzi wa muzuri—umusikilize Mungu.Upitishe wakati pamoja na Mashahidi wa Yehova; watakusaidia umukaribie Mungu.
Uendelee kujifunza juu ya Mungu na ujikaze kufuata amri zake.
Wakati imani yako inakuwa yenye nguvu, unapaswa kutoa maisha yako kwa Yehova na kubatizwa.—Matayo 28:19.
Umusikilize Mungu. Usome Biblia, na uombe Mashahidi wa Yehova wakusaidie ili uielewe ao kuisikia muzuri. Kisha utumie mu maisha yako mambo yenye unajifunza. Kama unafanya vile, utaishi milele.—Zaburi 37:29.