Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Yakobo

Mfano wa Kuigwa—Yakobo

Mfano wa Kuigwa​—Yakobo

Yakobo na ndugu yake, Esau, hawajasemezana kwa miaka mingi. Isitoshe, Esau anamchukia Yakobo. Ijapokuwa Yakobo hajafanya kosa lolote, ndiye anayechukua hatua ya kuziba pengo lililopo kati yao. Anasalimu amri. Lengo lake si kushinda mabishano bali kurudisha hali nzuri kati yake na ndugu yake. Yakobo halegezi msimamo wake, hata hivyo, hasisitizi Esau amwombe msamaha kabla ya kufanya amani naye.—Mwanzo 25:27-34; 27:30-41; 32:3-22; 33:1-9.

Ugomvi unapotokea katika familia yenu, wewe hufanya nini? Huenda nyakati nyingine ukahisi kwamba huna kosa hata kidogo na kwamba bila shaka, ndugu au dada yako au hata mzazi wako ndiye mwenye kosa. Katika hali kama hizo, unaketi kitako na kungoja mpaka wao wachukue hatua? Au unaweza kufuata mfano wa Yakobo? Ikiwa hakuna kanuni ya Biblia inayovunjwa, uko tayari kusalimu amri ili kuwe na amani? (1 Petro 3:8, 9) Yakobo hakuruhusu kiburi kigawanye familia yao. Alijinyenyekeza mbele ya ndugu yake nao wakafanya amani. Je, wewe, utafanya hivyo pia?