Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Ayubu

Mfano wa Kuigwa—Ayubu

Mfano wa Kuigwa​—Ayubu

Maisha ya Ayubu yamebadilika kabisa. Kwanza, amepoteza mali zake zote. Pili, watoto wake wamekufa. Tatu, amekuwa mgonjwa sana. Yote hayo yametokea ghafula. Akiwa amekata tamaa, Ayubu asema: “Nafsi yangu inahisi kuchukizwa na uhai wangu.” Asema kuwa ‘amejawa sana na aibu na kujawa na mateso.’ (Ayubu 10:1, 15) Hata hivyo, ijapokuwa ana dhiki, Ayubu hajamwacha Muumba wake. (Ayubu 2:10) Mabadiliko maishani mwake hayajambadili. Hivyo basi, Ayubu ni mfano mzuri wa uvumilivu.

Unapokumbwa na matatizo, huenda wewe pia ‘ukachukizwa na uhai wako.’ Hata hivyo, kama Ayubu, unaweza kuwa mtu asiyebadilika hata maisha yakibadilika, mtu ambaye ameazimia kabisa kumtumikia Yehova Mungu bila kuyumba-yumba. Yakobo aliandika: “Tazama! Tunawatangaza kuwa wenye furaha wale ambao wamevumilia. Mmesikia juu ya uvumilivu wa Ayubu nanyi mmeona matokeo ambayo Yehova alileta, kwamba Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.” (Yakobo 5:11) Alimjali Ayubu, naye anakujali wewe!