Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Musa

Mfano wa Kuigwa—Musa

Mfano wa Kuigwa​—Musa

Musa ana baraka nyingi maishani. Alilelewa katika nyumba ya kifalme ya Farao na kuelimishwa hekima yote ya Misri. (Matendo 7:22) Atautumia jinsi gani ujuzi huo? Anaweza kupata umashuhuri, mali, na mamlaka. Hata hivyo, hashawishiwi na marafiki wala kushawishiwa na tamaa ya kujitafutia makuu. Badala yake, anachagua kufanya kazi ambayo bila shaka inawashangaza wengi. Anaamua “kutendewa vibaya pamoja na watu wa Mungu.” (Waebrania 11:25) Je, Musa anakosa chochote? Hapana. Kwa sababu ya kuchagua kumtumikia Mungu na kuwasaidia watu, anafurahia maisha mazuri na yenye kuridhisha.

Ikiwa una nafasi ya kupata elimu nzuri ya msingi, utaitumia jinsi gani? Unaweza kufuatia pesa au mamlaka. Au, kama Musa unaweza kutumia maisha yako kwa njia inayofaa kwelikweli. Unaweza kutumia nguvu zako za kiakili na za kimwili kumtumikia Mungu na jirani zako. (Mathayo 22:35-40) Hakuna njia nyingine ya maisha yenye kuridhisha kama hiyo!