Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Timotheo

Mfano wa Kuigwa—Timotheo

Mfano wa Kuigwa​—Timotheo

Timotheo anakaribia kuondoka nyumbani—si kwamba anaitoroka familia yao lakini anaondoka ili kuandamana na mtume Paulo katika utumishi wa umishonari! Inaelekea Timotheo anakaribia umri wa miaka 20, na tayari yeye ni mwanamume kijana mwenye kuchukua mambo kwa uzito ambaye ‘ameshuhudiwa vema na akina ndugu katika Listra na Ikoniamu.’ (Matendo 16:2) Paulo ana hakika kwamba Timotheo anaweza kutimiza mambo makubwa katika utumishi wa Mungu. Na ndivyo inavyokuwa! Katika miaka inayofuata, Timotheo anasafiri sana ili kuanzisha makutaniko na kuwajenga akina ndugu. Sifa nzuri za Timotheo zinamvutia Paulo, ambaye miaka 11 hivi baadaye anawaambia Wafilipi: “Sina mtu mwingine yeyote aliye na mwelekeo kama wake atakayejali kwa unyoofu mambo yenu.”—Wafilipi 2:20.

Je, unajitoa ili kutumika katika utumishi wa Mungu? Ikiwa unafanya hivyo, kuna baraka nyingi mbele yako! Yehova anawathamini sana vijana ‘wanaojitoa kwa hiari.’ (Zaburi 110:3) Isitoshe, unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova Mungu ‘hakosi kuwa mwadilifu hivi kwamba aisahau kazi yako.’—Waebrania 6:10.