Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu Yafanyayo Kazi!

Majibu Yafanyayo Kazi!

DIBAJI

Majibu Yafanyayo Kazi!

‘Ninawezaje kupashana habari na wazazi wangu?’ ‘Ninaweza kupataje marafiki?’ ‘Ubaya wa kufanya ngono bila kuwajibika ni nini?’ ‘Kwa nini nina huzuni nyakati zote?’

Ikiwa umejiuliza maswali kama hayo, huko peke yako. Ikitegemea mahali ambapo umetafuta majibu ya maswali hayo, huenda umepata majibu yenye kutatanisha. Ili kuwasaidia vijana wapate mashauri thabiti yenye kutege- meka, gazeti la Amkeni! lilianzisha mfululizo wa makala zinazotegemea Biblia zenye kichwa “Vijana Huuliza . . . ” mnamo Januari 1982. Makumi ya miaka baadaye, makala hizo zingali zinawavutia wengi. Kila makala imefanyiwa utafiti mwingi. Ili kujua jinsi vijana wanavyofikiri na kuhisi, waandikaji wa Amkeni! wamezungumza na mamia ya vijana ulimwenguni pote! Zaidi ya yote, mashauri yanayotolewa katika makala hizo za “Vijana Huuliza” yanategemea Neno la Mungu, Biblia.

Kitabu ulicho nacho sasa hivi kilichapishwa mwanzoni mwaka wa 1989. Hata hivyo, sura hizo zimehaririwa upya ili kushughulikia masuala yanayowahangaisha vijana wa leo. Sura zipatazo 30 zimetokana na makala za “Vijana Huuliza” zilizochapishwa kati ya mwaka wa 2004 na 2011.

Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1, kitakusaidia kuwa mtu mzima mwenye kuwajibika. Tunatumaini kwamba kadiri unavyoyatumia mashauri yaliyomo, utajiunga na mamilioni ya vijana na watu wazima, ambao “nguvu zao za ufahamu zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.”​—Waebrania 5:14.

Wachapishaji