Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jalada la Ndani

Jalada la Ndani

Jalada la Ndani

Vijana Wapendwa,

Baba yenu wa mbinguni, Yehova Mungu, anawapenda sana. Anataka muwe na furaha. Huenda ukauliza: ‘Lakini inawezekana kuwa na furaha leo?’ Hilo ni swali zuri kwa kuwa tunakumbwa na matatizo mengi maishani. Ni kana kwamba kila siku tunapata matatizo yanayoweza kufanya tusiwe na furaha. Hata hivyo, Baba yetu mwenye upendo atatusaidia! Neno lake linatupatia mwongozo tunaohitaji ili kushughulikia matatizo maishani. Ingawa Biblia iliandikwa zamani sana, mashauri yaliyomo yanatumika leo kama vile tu wakati ilipoandikwa.—Zaburi 119:98, 99; 2 Timotheo 3:16, 17.

Tumepanga kitabu hiki kitayarishwe kwa sababu tunawapenda. Tunataka muwe na furaha kabisa maishani. Kwa hiyo, tunawatia moyo msome kitabu hiki kuanzia mwanzo hadi mwisho na pia mkirejelee kila wakati matatizo yanapotokea. Kusudi moja la kitabu hiki ni kuboresha mazungumzo kati yenu na wazazi wenu. Tunatumaini kwamba mtakisoma au hata kujifunza sehemu fulani pamoja. Faidikeni kutokana na hekima na ujuzi wa wazazi wenu!

Tunawatakia mema,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova