Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mapenzi ya Mungu Ni Nini?

Mapenzi ya Mungu Ni Nini?

Mungu anataka tuishi milele kwa amani na furaha katika paradiso duniani!

Huenda ukajiuliza, ‘Inawezekanaje?’ Biblia inasema kwamba Ufalme wa Mungu utafanya jambo hilo liwezekane, na ni mapenzi ya Mungu kwamba watu wote wajifunze kuhusu Ufalme huo na kusudi lake.—Zaburi 37:11, 29; Isaya 9:7.

Mungu anataka tunufaike.

Kama vile baba mzuri anavyowatakia watoto wake mema, Baba yetu wa mbinguni anataka tuishi milele kwa furaha. (Isaya 48:17, 18) Ameahidi kwamba yule “anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”—1 Yohana 2:17.

Mungu anataka tutembee katika njia zake.

Biblia inasema kwamba Muumba wetu anataka ‘kutufundisha njia zake’ ili ‘tutembee katika vijia vyake.’ (Isaya 2:2, 3) Amewapanga “watu kwa ajili ya jina lake” ili watangaze mapenzi yake duniani kote.—Matendo 15:14.

Mungu anataka tumwabudu kwa umoja.

Badala ya kuwagawanya watu, ibada safi ya Yehova huwaunganisha pamoja katika upendo wa kweli. (Yohana 13:35) Ni nani leo ambao wanawafundisha wanaume na wanawake kila mahali jinsi ya kumtumikia Mungu kwa umoja? Tunakutia moyo usome broshua hii ili upate jibu.