Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mapenzi ya Mungu Ni Nini?

Mapenzi ya Mungu Ni Nini?

Mungu anapenda tuishi milele katika amani na furaha mu paradiso ku dunia!

Lakini, unaweza kujiuliza hivi: ‘Hilo litawezekana namna gani?’ Biblia inasema kama ni Ufalme wa Mungu njo utafanya vile. Tena, Mungu anapenda watu wote wajifunze juu ya Ufalme huo, na wajue kusudi lake juu ya wanadamu.​—Zaburi 37:11, 29; Isaya 9:7.

Mungu anapenda tukuwe na maisha ya muzuri.

Kama vile baba muzuri anapenda watoto wake wakuwe na maisha ya muzuri, Baba yetu wa mbinguni anapenda tuishi milele katika furaha. (Isaya 48:17, 18) Ametoa ahadi (ao malako) kama “ule mwenye anafanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”​—1 Yohana 2:17.

Mungu anapenda tutembee katika njia zake.

Biblia inasema kama Muumbaji wetu anapenda ‘kutufundisha njia zake’ ili ‘tutembee katika mapito yake.’ (Isaya 2:2, 3) Amepanga muzuri “watu kwa ajili ya jina lake” ili wajulishe wengine mapenzi yake mu dunia yote.​—Matendo 15:14.

Mungu anapenda tumuabudu katika umoja.

Ibada safi ya Yehova hailete mugawanyiko kati ya watu, lakini inawafanya wakuwe na umoja, na wapendane kabisa. (Yohana 13:35) Leo, ni nani wako wanafundisha watu mu dunia yote namna ya kumutumikia Mungu katika umoja? Tunakuomba usome broshua hii ili upate jibu.