Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 1

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Namna Gani?

Denmaki

Taiwan

Venezuela

India

Unajua Mashahidi wa Yehova ngapi? Pengine wamoja kati yetu ni majirani wako, wafanyakazi wenzako, ao wanafunzi wenzako. Ao pengine tumekwisha kuzungumuza na wewe juu ya Biblia. Kwa kweli, sisi ni nani, na juu ya nini tunazungumuzaka na wengine juu ya mambo yenye tunaamini?

Tuko kama watu wengine. Tunatoka mu desturi mbalimbali, na tuko na hali mbalimbali za maisha. Wamoja kati yetu walikuwa mu dini ingine zamani, na wengine hawakukuwa wanamuamini Mungu. Lakini, mbele ya kuwa Mashahidi, sisi wote tulikamata wakati wa kuchunguza muzuri mafundisho ya Biblia. (Matendo 17:11) Tuliona kama mambo yenye tulijifunza ni ya kweli, na kwa hiyo kila mumoja wetu aliamua yeye mwenyewe kumuabudu Yehova Mungu.

Kujifunza Biblia kunatuletea faida. Sisi pia tuko na magumu na uzaifu kama watu wengine. Lakini, juu tunajikaza kutumia kanuni za Biblia mu maisha yetu ya kila siku, maisha yetu imebadilika na imekuwa muzuri zaidi. (Zaburi 128:1, 2) Ile ni sababu moja kati ya sababu zenye zinatuchochea tuambie wengine juu ya mambo ya muzuri yenye tumejifunza mu Biblia.

Tunafuata kanuni za Mungu mu maisha yetu. Kanuni hizo zenye zinapatikana mu Biblia, zinatusaidia kuwa na hali ya muzuri, kuheshimia watu wengine, na kuonyesha sifa mbalimbali kama vile unyoofu ao uaminifu na wema. Kanuni hizo zinatusaidia ili tukuwe na afya ya muzuri na tukuwe wanainchi wazuri, na zinasaidia familia zetu zikuwe na umoja na mwenendo muzuri. Juu tunaamini kabisa kama “Mungu hana ubaguzi,” tunajiona kuwa familia moja ya ndugu na dada mu dunia yote, hatuna ubaguzi wa rangi ya ngozi, na hatuache mambo ya politike itugawanye. Hata kama tuko kama watu wengine, familia yetu ya ndugu na dada mu dunia yote ni ya pekee.​—Matendo 4:13; 10:34, 35.

  • Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wako kama watu wengine?

  • Mashahidi wamejifunza kanuni gani mu Biblia?