Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 2

Kwa Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?

Kwa Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?

Noa

Abrahamu na Sara

Musa

Yesu Kristo

Watu wengi wanafikiri kwamba Mashahidi wa Yehova ni jina la dini mpya. Hata hivyo, zaidi ya miaka 2,700 iliyopita, watumishi wa Mungu wa pekee wa kweli waliitwa “mashahidi” wake. (Isaya 43:10-12) Kabla ya mwaka wa 1931, tulikuwa tukiitwa Wanafunzi wa Biblia. Kwa nini basi tulianza kutumia jina Mashahidi wa Yehova?

Jina hilo linamtambulisha Mungu wetu. Kulingana na maandishi ya kale, jina la Mungu, Yehova, linapatikana mara elfu kadhaa katika Biblia. Katika tafsiri nyingi jina hilo limeondolewa na badala yake majina ya cheo, kama vile Bwana au Mungu, yametumiwa. Hata hivyo, Mungu alijifunua kwa Musa akitumia jina lake binafsi, Yehova, na kusema: “Hilo ndilo jina langu milele.” (Kutoka 3:15) Jina hilo linamtofautisha na miungu yote ya uwongo. Tunajivunia kuitwa kwa jina takatifu la Mungu.

Jina hilo linafafanua kazi yetu. Watu wengi katika nyakati za kale, kuanzia Abeli aliyekuwa mwadilifu, walitoa ushahidi kuhusu imani yao katika Yehova. Kwa muda mrefu, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Daudi, na wengineo walijiunga na hilo “wingu kubwa . . . la mashahidi.” (Waebrania 11:4–12:1) Kama vile mtu anavyoweza kutoa ushahidi mahakamani ili kumtetea mtu asiye na hatia, sisi pia tumeazimia kutangaza ukweli kumhusu Mungu.

Tunapotumia jina hilo tunamwiga Yesu. Biblia inamwita “shahidi mwaminifu na wa kweli.” (Ufunuo 3:14) Yesu mwenyewe alisema kwamba ‘alilijulisha jina la Mungu’ naye akaendelea ‘kutoa ushahidi kuhusu kweli.’ (Yohana 17:26; 18:37) Hivyo, wafuasi wa kweli wa Kristo, wanaitwa kwa jina la Yehova, nao huwajulisha watu jina hilo. Hilo ndilo jambo ambalo Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kufanya.

  • Kwa nini Wanafunzi wa Biblia walianza kuitwa Mashahidi wa Yehova?

  • Yehova amekuwa na mashahidi duniani kwa muda gani?

  • Ni nani aliye Shahidi mkuu wa Yehova?