Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 2

Juu ya Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?

Juu ya Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?

Noa

Abrahamu na Sara

Musa

Yesu Kristo

Watu wengi wanawaza kama Mashahidi wa Yehova ni jina la dini ya mupya. Lakini, miaka zaidi ya 2 700 yenye imepita, Mungu wa kweli aliita watumishi wake kuwa “mashahidi” wake. (Isaya 43:10-12) Mbele ya mwaka wa 1931, tulikuwa tunaitwa Wanafunzi wa Biblia. Juu ya nini tulikamata jina Mashahidi wa Yehova?

Jina hilo linaonyesha Mungu wetu ni nani. Jina la Mungu, Yehova, linapatikana mara 7 000 hivi katika maandishi ya zamani ya Biblia. Mu tafsiri za mingi za Biblia wameondoa jina hilo, na nafasi ya jina hilo wametia majina ya cheo ao ya heshima, kama vile Bwana ao Mungu. Lakini Mungu wa kweli yeye mwenyewe njo alimuambia Musa kama jina lake ni Yehova. Alimuambia Musa hivi: “Hilo ndilo jina langu milele.” (Kutoka 3:15) Jina hilo linaonyesha kama iko tofauti na miungu yote ya uongo. Tuko wenye furaha sana juu tunaitwa kwa jina takatifu la Mungu.

Jina hilo linaonyesha kazi yetu. Watu wengi wa zamani, kuanzia Abeli mutu mwenye haki, walimuamini Yehova na walitoa ushahidi juu yake. Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Daudi, na wengine walijiunga na “wingu [hilo] kubwa la mashahidi.” (Waebrania 11:4–12:1) Kama vile tu mutu anaweza kutoa ushahidi kwenye tribinali ili kutetea mutu fulani mwenye hana kosa, sisi pia hatutaacha kuelezea wengine kweli juu ya Mungu wetu.

Tunafuata mufano wa Yesu. Biblia inaita Yesu “shahidi muaminifu na wa kweli.” (Ufunuo 3:14) Yesu mwenyewe alisema kama ‘alijulisha jina la Mungu’ na aliendelea ‘kutoa ushahidi juu ya ile kweli’ kuhusu Mungu. (Yohana 17:26; 18:37) Kwa hiyo, wanafunzi wa kweli wa Kristo wanapaswa kuitwa kwa jina la Yehova na kujulisha watu wengine jina hilo. Mashahidi wa Yehova wanajikaza kufanya vile.

  • Juu ya nini Wanafunzi wa Biblia walikamata jina Mashahidi wa Yehova?

  • Yehova amekuwa na mashahidi hapa ku dunia kuanzia wakati gani?

  • Ni nani mwenye kuwa Shahidi mukubwa zaidi wa Yehova?