Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 3

Namna Gani Kweli ya Biblia Ilipatikana Tena?

Namna Gani Kweli ya Biblia Ilipatikana Tena?

Wanafunzi wa Biblia, mu miaka ya 1870

Gazeti la kwanza la Munara wa Mulinzi, mwaka wa 1879

Munara wa Mulinzi leo

Biblia ilisema mbele ya wakati kama kisha kifo cha Kristo, walimu wa uongo wangetokea kati ya Wakristo wa kwanza-kwanza na wangepotosha kweli ya Biblia. (Matendo 20:29, 30) Kisha wakati fulani, jambo hilo lilitokea kabisa. Walimu hao wa uongo walichanga mafundisho ya Yesu na mafundisho ya wapagani, na hilo likatokeza Ukristo wa uongo. (2 Timoteo 4:3, 4) Namna gani tunaweza kuwa hakika kama leo tunaelewa muzuri mambo yenye Biblia inafundisha kabisa?

Wakati ulifika ili Yehova afunue kweli. Yehova alitabiri kama katika ‘wakati wa mwisho ujuzi wa kweli ungekuwa mwingi.’ (Danieli 12:4) Mu mwaka wa 1870, kikundi kidogo cha watu wenye walikuwa wanatafuta kweli, walitambua kama mafundisho mingi ya dini haikupatana na Biblia. Kwa hiyo, walianza kujifunza Biblia ili waelewe mafundisho ya kweli ya Biblia, na Yehova aliwasaidia kuelewa maandiko.

Wanaume waaminifu walijifunza Biblia kwa uangalifu. Wanafunzi hao wa Biblia wenye bidii walikuwa wanatumia njia ya kujifunza yenye tunaendelea kutumia mupaka leo. Walikuwa wanajifunza fundisho moja la Biblia, wakati walikuwa wanamaliza fundisho hilo, walikuwa wanakamata fundisho lingine. Wakati ilikuwa nguvu kuelewa andiko fulani la Biblia, walikuwa wanatafuta maandiko ingine yenye kufasiria andiko hilo. Wakati walifikia uamuzi wenye kupatana na Maandiko ya Biblia, waliandika jambo hilo. Kwa kufanya vile, waliacha Biblia ijifasirie yenyewe. Kwa hiyo, walivumbua kweli juu ya jina la Mungu na Ufalme wake, kusudi lake juu ya wanadamu na dunia, hali ya watu wenye wamekufa, na tumaini la ufufuo. Kutafuta kweli mu Biblia kuliwasaidia waachane na mafundisho na desturi za mingi za uongo.​—Yohana 8:31, 32.

Kufikia mwaka wa 1879, Wanafunzi hao wa Biblia waliona kama wakati ulikuwa umefika wa kutangazia watu mafundisho ya kweli. Kwa hiyo, mu mwaka huo, walianza kuchapisha gazeti Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova, gazeti hilo linaendelea kuchapishwa mupaka leo. Sasa tunafundisha watu mafundisho ya kweli ya Biblia mu inchi 240 na mu luga zaidi ya 900. Leo ujuzi wa kweli ni mwingi sana kuliko wakati mwingine wowote!

  • Kisha kifo cha Kristo, kulitokea nini juu ya mafundisho ya kweli ya Biblia?

  • Ni nini imetusaidia kupata tena ile kweli ya Neno la Mungu?