Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 4

Kwa Nini Tumechapisha Tafsiri ya Ulimwengu Mpya?

Kwa Nini Tumechapisha Tafsiri ya Ulimwengu Mpya?

Kongo (Kinshasa)

Rwanda

Kisehemu cha tafsiri ya Kigiriki ya Symmachus cha karne ya tatu au ya nne kilicho na jina la Mungu kwenye Zaburi 69:31

Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova walitumia, wakachapisha, na kusambaza tafsiri mbalimbali za Biblia. Lakini tukaona uhitaji wa kuchapisha tafsiri mpya ya Biblia ambayo ingewasaidia zaidi watu wajifunze “ujuzi sahihi wa kweli,” na hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwa kila mtu. (1 Timotheo 2:3, 4) Hivyo, mwaka wa 1950 tukaanza hatua kwa hatua kuchapisha Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inayotumia lugha ya kisasa. Biblia hii imetafsiriwa kwa uaminifu na kwa usahihi katika lugha zaidi ya 130.

Biblia inayoeleweka kwa urahisi ilihitajiwa. Lugha hubadilika baada ya muda, na tafsiri nyingi za Biblia zina maneno ambayo hayatumiki tena au hayaeleweki kwa urahisi. Pia, maandishi ya kale ambayo ni sahihi zaidi na ambayo yaliandikwa muda mfupi baada ya nakala za kwanza kuandikwa yamepatikana na hivyo kufanya iwezekane kuelewa vizuri zaidi Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki kilichotumiwa kuandika Biblia.

Tafsiri ambayo haipotoshi neno la Mungu ilihitajiwa. Badala ya kubadili maandishi yaliyoongozwa na roho ya Mungu, watafsiri wa Biblia wanapaswa kutafsiri maandishi ya awali kwa uaminifu. Hata hivyo, katika tafsiri nyingi, jina la Mungu, Yehova, halipatikani katika Maandiko Matakatifu.

Biblia ambayo inamheshimu Mtungaji wake ilihitajiwa. (2 Samweli 23:2) Katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, jina la Yehova limerudishwa kila mahali ambapo jina hilo linapatikana mara 7,000 hivi katika maandishi ya zamani zaidi ya Biblia, kama inavyoonyeshwa katika picha iliyo hapa chini. (Zaburi 83:18) Kwa sababu ya utafiti uliofanywa kwa makini kwa miaka mingi, utafurahia kuisoma Biblia hii, kwa kuwa inaeleza mawazo ya Mungu waziwazi. Iwe una Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika lugha yako au la, tunakutia moyo uwe na mazoea ya kusoma Neno la Yehova kila siku.—Yoshua 1:8; Zaburi 1:2, 3.

  • Kwa nini tuliamua kwamba tafsiri mpya ya Biblia inahitajiwa?

  • Kila mtu anayetaka kujifunza mapenzi ya Mungu anapaswa kuwa na mazoea ya kufanya nini kila siku?