Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 4

Juu ya Nini Tulikuwa na Lazima ya Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya?

Juu ya Nini Tulikuwa na Lazima ya Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya?

Congo (Kinshasa)

Rwanda

Maandishi ya Symmachus (miaka 300 ao 400 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu) yenye kuwa na jina la Mungu katika Zaburi 69:31.

Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova walitumia tafsiri mbalimbali za Biblia, walichapisha tafsiri hizo, na walizigawia watu. Lakini tuliona kama, ili kusaidia muzuri watu wapate “ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli,” wenye Mungu anapenda kila mutu apate, iliomba kuwa na tafsiri ya mupya ya Biblia. (1 Timoteo 2:3, 4) Kwa hiyo, mu mwaka wa 1950 tulianza kutoa sehemu za Biblia yetu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya yenye kutumia luga ya sasa. Biblia hiyo imetafsiriwa kwa uaminifu na bila makosa mu luga zaidi ya 170.

Tulikuwa na lazima ya tafsiri ya Biblia yenye kuwa mwepesi kuelewa ao kusikia muzuri. Luga zinabadilikaka kisha wakati fulani, na Biblia za mingi ziko na maneno yenye haiko wazi ao ya zamani yenye kuwa nguvu kuelewa. Tena, maandishi ya zamani ya Biblia yenye haina makosa na yenye kukaribia maandishi ya kwanza-kwanza imevumbuliwa. Ile maandishi imesaidia kuelewa muzuri Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki chenye kilitumiwa ili kuandika Biblia.

Tulikuwa na lazima ya tafsiri yenye haibadilishe neno la Mungu. Kuliko kubadilisha maandishi yenye iliongozwa na roho ya Mungu, watafsiri wa Biblia wanapaswa kufuata kwa uaminifu maandishi ya kwanza-kwanza. Lakini, tafsiri za mingi za Biblia hazitumie jina la Mungu, Yehova.

Tulikuwa na lazima ya tafsiri ya Biblia yenye inamutukuza ule mwenye aliandikisha Biblia. (2 Samweli 23:2) Kama vile mufano wenye kuwa hapa chini unaonyesha, mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, jina Yehova limerudishwa nafasi kwenye lilikuwa mu maandishi ya zamani ya Biblia, ni kusema, mara 7 000 hivi. (Zaburi 83:18) Kwa sababu wale wenye walitafsiri Biblia hiyo walitafuta habari kwa bidii na kwa miaka mingi, mutu anasikiaka furaha wakati iko anaisoma juu inaonyesha waziwazi mawazo ya Mungu. Ikuwe uko na Tafsiri ya Ulimwengu Mupya mu luga yako ao hapana, tunakutia moyo kusoma Neno la Yehova kila siku.​—Yoshua 1:8; Zaburi 1:2, 3.

  • Juu ya nini tulikuwa na lazima ya tafsiri ya mupya ya Biblia?

  • Kila mutu mwenye anapenda kujua mapenzi ya Mungu anapaswa kufanya nini kila siku?