Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 6

Tunafaidikaje kwa Kushirikiana na Wakristo Wenzetu?

Tunafaidikaje kwa Kushirikiana na Wakristo Wenzetu?

Madagaska

Norway

Lebanoni

Italia

Hata ikitulazimu kusafiri kupitia msitu mkubwa au hali ya hewa ikiwa mbaya, tunahudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida. Kwa nini Mashahidi wa Yehova wanajitahidi sana kushirikiana na waamini wenzao, licha ya kwamba huenda wakawa na hali ngumu maishani au uchovu baada ya kufanya kazi siku nzima?

Ni kwa faida yetu. Paulo, alipokuwa akizungumzia wale tunaoshirikiana nao katika kutaniko, alisema “tufikiriane.” (Waebrania 10:24) Neno hilo linamaanisha ni lazima tujuane vizuri. Hivyo, tunatiwa moyo tuwajali wengine. Tunapoendelea kuwafahamu Wakristo wenzetu, tunatambua kwamba baadhi yao wamekabili na kushinda hali fulani ngumu kama yetu na wanaweza kutusaidia ili sisi pia tufaulu.

Hufanya tuwe na urafiki wa kudumu. Akina ndugu na dada ambao tunakutanika pamoja nao katika mikutano yetu ni rafiki zetu wa karibu, si watu tunaowafahamu tu. Pindi nyingine, tunashirikiana nao katika tafrija. Tunapata faida gani kwa kushirikiana nao kwa njia hizo? Tunajifunza kuwathamini wengine hata zaidi, na jambo hilo linaimarisha upendo kati yetu. Kisha, wenzetu wanapokumbwa na matatizo, tunakuwa tayari kuwasaidia kwa sababu tayari tumejenga urafiki wenye upendo kati yetu. (Methali 17:17) Kwa kushirikiana na wote kutanikoni, tunaonyesha kwamba ‘tunatunzana.’—1 Wakorintho 12:25, 26.

Tunakutia moyo uchague marafiki wanaofanya mapenzi ya Mungu. Utapata marafiki hao miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Usiruhusu kitu chochote kikuzuie kushirikiana nasi.

  • Kwa nini ni muhimu kwetu kushirikiana pamoja kwenye mikutano?

  • Ungependa kuanza lini kuhudhuria mikutano yetu?