Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 6

Kupitisha Wakati Pamoja na Ndugu na Dada Zetu Kunatuletea Faida Gani?

Kupitisha Wakati Pamoja na Ndugu na Dada Zetu Kunatuletea Faida Gani?

Madagaska

Norvège

Lebanoni

Italia

Hata kama tunapaswa kupita mu pori, hata kama kuko mvua, baridi ao jua kali, tunaenda ku mikutano yetu kila mara. Hata kama tuko na magumu, ao hata kama tunachoka kisha kazi, juu ya nini sisi Mashahidi wa Yehova tunajikaza kukutana pamoja na ndugu na dada zetu?

Kunatusaidia tukuwe na hali ya muzuri. Mutume Paulo alitia moyo ndugu na dada katika makutaniko ‘wafikiriane.’ (Waebrania 10:24) Neno hilo linamaanisha kama tunapaswa kujuana muzuri. Kwa hiyo, mutume Paulo anatutia moyo tuhangaikie ndugu na dada zetu. Wakati tunajua muzuri familia zingine za Wakristo wenzetu, tunavumbua kama wamoja kati yao wameshinda magumu yenye kufanana na yetu na wanaweza kutusaidia na sisi tushinde magumu yetu.

Kunatusaidia tupate marafiki wa kweli. Ku mikutano yetu, tunakutana pamoja na ndugu na dada zetu wenye kuwa marafiki wetu kabisa, hatuwaone tu kuwa watu wenye tunajuana nao. Wakati mwingine, tunakutana nao ili kujifurahisha kwa njia yenye kufaa. Kufanya vile kunatuletea faida gani? Kunatusaidia tuone ndugu na dada zetu kuwa watu wa maana, na kunafanya tuwapende zaidi. Kwa hiyo, wakati wanapata magumu, tuko tayari kuwasaidia juu wamekuwa marafiki wetu wa sana. (Mezali 17:17) Wakati tunafanya urafiki pamoja na ndugu na dada wote wa kutaniko letu, tunaonyesha kama ‘tunahangaikiana.’​—1 Wakorinto 12:25, 26.

Tunakutia moyo uchague marafiki wako kati ya watu wenye wanafanya mapenzi ya Mungu. Utapata marafiki wa namna ile kati ya Mashahidi wa Yehova. Tafazali, usiache hata kitu kimoja kikuzuie kupitisha wakati pamoja na sisi.

  • Tunapata faida gani wakati tunapitisha wakati pamoja na ndugu na dada zetu ku mikutano?

  • Utakuja ku mikutano yetu wakati gani?