Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 7

Mikutano Yetu Inafanywa Namna Gani?

Mikutano Yetu Inafanywa Namna Gani?

Nouvelle-Zélande

Japani

Uganda

Lituania

Wakati Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanafanya mikutano yao, sehemu kubwa ya mikutano yao ilikuwa kuimba, kusali, na kusoma Maandiko na kuizungumuzia. Hawakufanya desturi zingine za dini. (1 Wakorinto 14:26) Wakati wa mikutano yetu, sisi pia tunafanyaka vile.

Mafundisho yetu inatoka mu Biblia na inatusaidia mu maisha. Siku ya Posho ao Siku ya Yenga, ndugu na dada wa kila kutaniko wanakutana ili kusikiliza hotuba yenye kutegemea Biblia ya dakika 30. Hotuba hiyo inaonyesha namna Maandiko inaweza kutusaidia mu maisha na inatusaidia kujua mambo yenye Maandiko inasema juu ya wakati wetu. Wakati musemaji anasoma maandiko, sisi wote tunatiwa moyo kufuatana naye mu Biblia zetu. Kisha hotuba, tunafanya Funzo la “Munara wa Mulinzi” kwa saa moja. Tunazungumuzia habari fulani yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi gazeti la funzo, na kila mutu anaweza kutoa majibu. Ile mazungumuzo inatusaidia kujua namna ya kutumia mashauri ya Biblia mu maisha yetu. Mashahidi wa Yehova wanajifunza habari ileile mu makutaniko zaidi ya 120 000 mu dunia yote.

Mikutano inatusaidia kufanya ufundi wetu wa kufundisha ukuwe muzuri zaidi. Katikati ya juma, tunakutana pia siku fulani ili kufuata mukutano wenye kuwa na sehemu tatu wenye kuitwa Utumishi na Maisha ya Mukristo. Habari za mukutano huo zinapatikana mu Buku la Mukutano Utumishi na Maisha lenye kutolewa kila mwezi. Sehemu ya kwanza ya mukutano huo inaitwa Utajiri wa Neno la Mungu; inatusaidia kuelewa muzuri sehemu fulani ya Biblia yenye kutaniko liliombwa kusoma mbele ya wakati. Sehemu ya pili yenye kuitwa Tujitoe Kabisa Katika Kazi ya Kuhubiri, iko na maonyesho yenye kutusaidia kujua namna ya kuzungumuza na watu juu ya habari zenye kuwa mu Biblia. Kuko mushauri mwenye kufuata kwa uangalifu migao hiyo na kisha anatoa mashauri yenye kutusaidia kufanya ufundi wetu wa kusoma na kuzungumuza ukuwe muzuri zaidi. (1 Timoteo 4:13) Sehemu ya mwisho inaitwa Maisha ya Mukristo; inatusaidia tujue namna ya kutumia kanuni za Biblia mu maisha yetu ya kila siku. Inatia ndani mazungumuzo ya maulizo na majibu yenye inatusaidia tuelewe Biblia muzuri zaidi.

Wakati utakuja ku mikutano yetu, kwa kweli utafurahia mafundisho ya muzuri sana ya Biblia yenye utapata kule.​—Isaya 54:13.

  • Utasikia mambo gani ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova?

  • Kati ya mikutano yenye tunafanya kila juma, ungependa kuja ku mukutano gani?