Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 8

Kwa Nini Tunavalia Vizuri Tunapohudhuria Mikutano?

Kwa Nini Tunavalia Vizuri Tunapohudhuria Mikutano?

Iceland

Mexico

Guinea-Bissau

Filipino

Katika picha za broshua hii, je, umeona jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyovalia vizuri wanapohudhuria mikutano? Kwa nini tunachukua kwa uzito jinsi tunavyovalia na kujipamba?

Ili kuonyesha kwamba tunamheshimu Mungu wetu. Ni kweli kwamba Mungu hakazii fikira jinsi tulivyo kwa nje. (1 Samweli 16:7) Hata hivyo, tunapokutanika pamoja, tamaa yetu kuu ni kumwonyesha Mungu heshima na pia waabudu wenzetu. Ikiwa ungemtembelea mfalme au rais, bila shaka ungevalia kwa heshima kwa sababu ya cheo chake. Vivyo hivyo, tunapovalia vizuri katika mikutano, tunamheshimu “Mfalme wa mataifa,” Yehova Mungu, na pia mahali tunapomwabudia.—Yeremia 10:7.

Ili kuonyesha viwango tunavyofuata maishani. Biblia inawatia moyo Wakristo wavalie kwa “kiasi na utimamu wa akili.” (1 Timotheo 2:9, 10) Kuvalia kwa “kiasi” kunamaanisha kuepuka mavazi ambayo yanaweza kuwafanya watu watukazie fikira kama vile mavazi ya kujionyesha, yanayoamsha tamaa mbaya, au yanayoonyesha uchi. Pia, kuwa na “utimamu wa akili” kunatusaidia kuchagua mavazi yenye kupendeza ambayo si ya kizembe au yanayopita kiasi. Kanuni hizi hazitubani, bado tuna uhuru wa kuchagua mavazi yanayotupendeza. Tunapovalia vizuri, ‘tunalipamba fundisho la Mwokozi wetu,’ na ‘kumtukuza Mungu.’ (Tito 2:10; 1 Petro 2:12) Hivyo, wengine wanaiheshimu ibada ya Yehova.

Si lazima mtu avae mavazi rasmi ili ahudhurie mikutano katika Jumba la Ufalme. Mavazi ya kawaida yanaweza kuwa safi, nadhifu, na yenye kufaa.

  • Kwa nini ni muhimu kuvalia vizuri tunapomwabudu Mungu?

  • Ni kanuni gani zinazotuongoza tunapochagua jinsi tunavyovalia na kujipamba?