Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 10

Ibada ya Familia Ni Nini?

Ibada ya Familia Ni Nini?

Korea Kusini

Brazili

Australia

Guinea

Kuanzia wakati wa zamani, Yehova anapenda watu wa kila familia wakuwe na wakati wa kujifunza pamoja ili wakuwe na urafiki wenye nguvu pamoja naye, na ili wakuwe na uhusiano wenye nguvu sana kati yao. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Njo maana, kila familia ya Mashahidi wa Yehova inapanga wakati fulani kila juma ili kumuabudu Yehova pamoja. Wakati huo, mu hali yenye kutulia, wanazungumuzia mambo ya kiroho yenye inapatana na mahitaji ya familia yao. Hata kama unaishi peke yako, unaweza kupanga wakati kama huo ili kumukaribia Mungu zaidi kwa kujifunza habari fulani ya Biblia yenye unapenda.

Ni wakati wa kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova. Biblia inasema hivi: “Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Tunamujua Yehova muzuri wakati tunajifunza mambo mingi juu ya sifa zake na matendo yake kupitia Biblia, Neno lake. Namna ya mwepesi ya kuanza ibada ya familia ni kusoma Biblia pamoja kwa sauti kubwa, pengine kwa kufuata programu ya kila juma ya Mukutano Utumishi na Maisha. Kila mutu wa familia anaweza kupewa sehemu ya kusoma, na kisha ninyi wote munaweza kuzungumuzia mambo yenye mumejifunza mu Maandiko.

Ni wakati wa kutia nguvu uhusiano kati ya watu wa familia. Bibi na bwana, pia wazazi na watoto, wanatia nguvu uhusiano kati yao wakati wanajifunza Biblia mu familia. Wakati wa ibada ya familia unapaswa kuwa wakati wa furaha na amani, wakati wenye kila mutu mu familia anangojea kwa hamu katika juma. Kupatana na miaka ya watoto wao, wazazi wanaweza kuchagua habari za kuzungumuzia zenye zinapatana na mahitaji ya watoto wao. Pengine wanaweza kutumia habari za Munara wa Mulinzi na Amuka! ao habari zenye kuwa ku site yetu ya Enternete, jw.org. Munaweza kuzungumuzia magumu yenye watoto walipata ku masomo na kuwasaidia wajue namna ya kupambana na ile magumu. Munaweza kuangalia programu ya JW Télédiffusion (tv.pr418.com) na kuizungumuzia pamoja. Munaweza kujifunza nyimbo zenye mutaimba ku mikutano, na munaweza kula ao kunywa kitu fulani kisha ibada ya familia.

Wakati huo wa maana wenye munapitisha pamoja kila juma ili kumuabudu Yehova, utasaidia kila mutu mu familia afurahie kujifunza Neno la Mungu, na Yehova atabariki sana bidii yenu.​—Zaburi 1:1-3.

  • Juu ya nini tunapanga wakati wa kufanya ibada ya familia?

  • Wazazi wanaweza kufanya nini ili kila mutu mu familia afurahie wakati huo?