Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 12

Kazi Yetu ya Kuhubiri Ufalme Inafanywa Namna Gani?

Kazi Yetu ya Kuhubiri Ufalme Inafanywa Namna Gani?

Uhispania

Belarusi

Hong Kong

Peru

Wakati mufupi mbele Yesu akufe, alisema hivi: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.” (Matayo 24:14) Lakini, kazi hiyo ya kuhubiri mu dunia yote ingefanywa namna gani? Kwa kuiga njia zenye Yesu alitumia ili kuhubiri wakati alikuwa ku dunia.​—Luka 8:1.

Tunahubiri nyumba kwa nyumba. Yesu alizoeza wanafunzi wake kuhubiri habari njema nyumba kwa nyumba. (Matayo 10:11-13; Matendo 5:42; 20:20) Wahubiri hao wa kwanza-kwanza walipewa maeneo ya kuhubiri. (Matayo 10:5, 6; 2 Wakorinto 10:13) Leo pia, kazi yetu ya kuhubiri inapangwa muzuri, na kila kutaniko linapewa eneo la kuhubiri. Hilo linatusaidia kutimiza amri ya Yesu ya ‘kuhubiria watu na kutoa ushahidi kamili.’​—Matendo 10:42.

Tunajikaza kuhubiria watu kila mahali kwenye wanaweza kupatikana. Yesu alituachia mufano mwingine; alikuwa anahubiria watu mahali pa watu wengi; kama vile pembeni ya bahari ao ku kisima kwenye watu wengi walikuwa wanakuja kushota maji. (Marko 4:1; Yohana 4:5-15) Sisi pia tunazungumuza na watu juu ya Biblia kila mahali kwenye wanaweza kupatikana kama vile ku barabara, nafasi za biashara ao kupitia telefone. Tena, wakati tunapata nafasi, tunahubiria majirani wetu, wafanyakazi wenzetu, wanafunzi wenzetu, na watu wa jamaa yetu. Kwa sababu tunajikaza kutumia njia hizo zote za kuhubiri, mamilioni ya watu mu dunia yote wamesikia “habari njema za wokovu.”​—Zaburi 96:2.

Kuko mutu fulani mwenye unaweza kuzungumuza naye juu ya habari njema ya Ufalme wa Mungu, na juu ya faida zenye atapata wakati wenye kuja kama anaisikiliza? Usikose kuambia wengine habari hiyo yenye kutolea watu tumaini. Ufanye vile wakati tu utapata nafasi!

  • Ni “habari njema” gani yenye inapaswa kuhubiriwa?

  • Namna gani Mashahidi wa Yehova wanaiga njia zenye Yesu alitumia ili kuhubiri?