Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 13

Painia Ni Nani?

Painia Ni Nani?

Kanada

Nyumba kwa nyumba

Funzo la Biblia

Funzo la kibinafsi

Mara nyingi, “painia” ni mtu anayevumbua maeneo mapya na njia ambayo wengine wanaweza kufuata. Tunaweza kusema kwamba Yesu alikuwa painia kwa sababu alitumwa duniani ili kuhudumu na kuwafungulia watu njia ya kupata wokovu. (Mathayo 20:28) Leo, wafuasi wake wanamwiga kwa kutumia muda mwingi iwezekanavyo katika kazi ya ‘kufanya wanafunzi.’ (Mathayo 28:19, 20) Wengine wamejiunga na utumishi unaoitwa upainia.

Painia ni mhubiri wa habari njema wa wakati wote. Mashahidi wote wa Yehova ni wahubiri wa habari njema. Hata hivyo, wengine wamepanga mambo yao ili wawe mapainia wa kawaida, wakitumia saa 70 kila mwezi katika kazi ya kuhubiri. Wengi wao wanachagua kufanya kazi ya muda. Huenda wengine wakachaguliwa kuwa mapainia wa pekee katika maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme, wakitumia saa 130 au zaidi katika huduma kila mwezi. Mapainia wanaridhika na mahitaji ya msingi, nao wana hakika kwamba Yehova atawaandalia mambo ya lazima maishani. (Mathayo 6:31-33; 1 Timotheo 6:6-8) Wale ambao hawawezi kuwa mapainia wa wakati wote wanaweza kuwa mapainia wasaidizi wanapoweza. Wanafanya hivyo kwa kuongeza utendaji wao wakihubiri saa 30 au 50 kwa mwezi.

Painia anachochewa na upendo wake kwa Mungu na watu. Kama Yesu, tunatambua kwamba watu wengi leo wana uhitaji mkubwa wa kiroho. (Marko 6:34) Lakini tuna ujuzi ambao unaweza kuwasaidia sasa, na kuwapa tumaini hakika la wakati ujao. Kumpenda jirani kunamchochea painia atumie kwa hiari wakati na nguvu zake kuwasaidia wengine kiroho. (Mathayo 22:39; 1 Wathesalonike 2:8) Anapofanya hivyo, imani yake inaimarishwa, anamkaribia zaidi Mungu, naye anakuwa na furaha nyingi.—Matendo 20:35.

  • Painia ni nani?

  • Ni nini kinachowachochea wengine wawe mapainia wa wakati wote?