Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 13

Painia Ni Nani?

Painia Ni Nani?

Kanada

Nyumba kwa nyumba

Funzo la Biblia

Funzo la pekee

Mara mingi “painia” ni mutu mwenye anaendaka kuangalia namna eneo fulani la mupya liko na kufungulia wengine njia ili waifuate. Tunaweza kusema kama Yesu alikuwa painia, juu alitumwa ku dunia ili kuhubiri ujumbe wenye kutoa uzima na kufungua njia ya kupata wokovu. (Matayo 20:28) Leo, wanafunzi wake wanafuata mufano wake kwa kufanya saa za mingi kadiri wanaweza mu kazi ya ‘kufanya wanafunzi.’ (Matayo 28:19, 20) Wamoja wameweza kufanya vile kwa kufanya kazi ya upainia.

Painia ni muhubiri wa wakati wote. Mashahidi wa Yehova wote ni wahubiri wa habari njema. Lakini, wamoja kati yao wamejipanga muzuri mu maisha yao ili wakuwe mapainia wa kawaida; wanahubiri saa 70 kila mwezi. Ili kufanya vile, wengi wanafanya kazi za kimwili zenye haziwakamate wakati wote. Wengine wanachaguliwa ili wakuwe mapainia wa pekee kusudi waende kutumikia mu maeneo yenye kuwa na lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme; wanahubiri saa 130 ao zaidi kila mwezi. Mapainia wanafurahia kuishi maisha mepesi, wako hakika kama Yehova atawatolea mambo ya lazima mu maisha. (Matayo 6:31-33; 1 Timoteo 6:6-8) Wale wenye hawawezi kuwa mapainia wa kawaida ao wa pekee, wanaweza kuwa mapainia wasaidizi wakati wanaweza kufanya vile; wanaongeza bidii yao kwa kuhubiri saa 30 ao 50 kwa mwezi.

Kupenda Mungu na watu njo kunachochea mutu akuwe painia. Kama Yesu, tunatambua kama watu wengi leo wako na lazima kabisa ya kumujua Mungu na makusudi yake. (Marko 6:34) Lakini mambo yenye tunajua inaweza kuwasaidia kuanzia leo, na kuwapatia tumaini juu ya wakati wenye kuja. Kupenda jirani njo kunamuchochea painia atumie wakati wake na nguvu zake ili kusaidia wengine wajue habari njema. (Matayo 22:39; 1 Watesalonike 2:8) Kwa hiyo, imani yake inatiwa nguvu, anamukaribia Yehova zaidi, na anapata furaha sana.​—Matendo 20:35.

  • Painia ni nani?

  • Ni nini inachochea wahubiri fulani wakuwe mapainia wa kawaida ao wa pekee?