Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 17

Waangalizi wa Mzunguko Wanatusaidiaje?

Waangalizi wa Mzunguko Wanatusaidiaje?

Malawi

Kikundi cha utumishi

Huduma ya shambani

Mkutano wa wazee

Biblia huwataja mara kadhaa Barnaba na mtume Paulo. Wanaume hao walikuwa waangalizi wanaosafiri, wakiyatembelea makutaniko ya karne ya kwanza. Kwa nini? Walihangaikia kikweli hali ya ndugu zao wa kiroho. Paulo alisema kwamba alitaka ‘kurudi akawatembelee akina ndugu’ ili aone jinsi wanavyoendelea. Alikuwa tayari kusafiri mamia ya kilometa kwenda kuwaimarisha. (Matendo 15:36) Hiyo ndiyo tamaa ya waangalizi wa mzunguko leo.

Wanakuja kututia moyo. Kila mwangalizi wa mzunguko hutembelea makutaniko 20 hivi. Yeye hukaa katika kila kutaniko kwa muda wa juma moja, mara mbili kila mwaka. Tunaweza kufaidika sana kutokana na uzoefu wa ndugu hao na wake zao pia, ikiwa wameoa. Wanajitahidi kuwafahamu vizuri vijana kwa wazee, nao wana hamu ya kuandamana pamoja nasi katika huduma ya shambani na kwa wale tunaojifunza nao Biblia. Waangalizi hao huandamana pamoja na wazee kufanya ziara za uchungaji. Ili kutuimarisha, wao hutoa hotuba zenye kutia moyo katika mikutano na makusanyiko.—Matendo 15:35.

Wanapendezwa na wote kutanikoni. Waangalizi wa mzunguko wanapendezwa sana na hali ya kiroho ya makutaniko. Wao hufanya mkutano pamoja na wazee na watumishi wa huduma ili kuzungumzia maendeleo ambayo yamefanywa na kuwapa mapendekezo kuhusu jinsi ya kushughulikia majukumu yao. Wanawasaidia mapainia kupata mafanikio katika huduma yao, nao hufurahia kuwajua wapya na kusikia kuhusu maendeleo yao ya kiroho. Kila mmoja wa ndugu hao hujitoa kwa hiari akiwa “mfanyakazi mwenzi kwa ajili ya faida [yetu].” (2 Wakorintho 8:23) Tunapaswa kuiga imani yao na roho yao ya kujitoa kufanya mapenzi ya Mungu.—Waebrania 13:7.

  • Kwa nini waangalizi wa mzunguko hutembelea makutaniko?

  • Unaweza kufaidika jinsi gani kutokana na ziara zao?