Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 17

Waangalizi wa Muzunguko Wanatusaidia Namna Gani?

Waangalizi wa Muzunguko Wanatusaidia Namna Gani?

Malawi

Kikundi cha mahubiri

Mahubiri

Mukutano wa wazee

Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo inazungumuzia mara mingi Barnaba na mutume Paulo. Wanaume hao walikuwa waangalizi wenye kusafiri; walikuwa wanatembelea makutaniko ya wakati wa mitume. Juu ya nini? Walihangaikia sana ndugu na dada zao, na walipenda wakuwe na hali ya muzuri. Mutume Paulo alisema kama alipenda ‘kurudia na kutembelea ndugu’ ili kuona wako namna gani. Alikuwa tayari kufanya safari ya murefu ili kuenda kuwatia nguvu. (Matendo 15:36) Leo pia, waangalizi wetu wenye kusafiri wanapenda sana kufanya vile.

Wanakuja kututia moyo. Kila mwangalizi wa muzunguko anatembelea makutaniko 20 hivi. Anatembelea kila kutaniko mara mbili kwa mwaka na anapitisha juma moja mu kila kutaniko. Tunaweza kupata faida kabisa kupitia uzoefu wa ndugu hao na uzoefu wa bibi zao ikiwa wamekwisha kuoa. Wanajikaza kujua vijana na watu wazima, na wanapenda kutusindikiza mu kazi ya kuhubiri na ya kuongoza mafunzo yetu ya Biblia. Waangalizi hao wanafanya kazi ya uchungaji pamoja na wazee, na wanatia imani yetu nguvu wakati wanatoa hotuba zenye kujenga ku mikutano na ku mikusanyiko.​—Matendo 15:35.

Wanahangaikia kila mumoja wetu. Waangalizi wa muzunguko wanahangaikia sana hali ya kiroho ya kutaniko. Wanafanya mukutano pamoja na wazee na watumishi wa huduma ili kuchunguza maendeleo ya kutaniko na kuwapatia mashauri yenye kufaa juu ya namna wanaweza kufanya kazi yao muzuri zaidi. Wanasaidia mapainia ili wakuwe na matokeo ya muzuri mu kazi yao ya kuhubiri, na wanafurahia kuona wapya wenye wamejiunga na tengenezo na kusikia habari juu ya maendeleo yao ya kiroho. Kila mwangalizi wa muzunguko anajitolea kuwa ‘mufanyakazi mwenzetu, kwa ajili ya faida yetu.’ (2 Wakorinto 8:23) Tunapaswa kuiga imani yao na ushikamanifu wao kwa Mungu.​—Waebrania 13:7.

  • Juu ya nini waangalizi wa muzunguko wanatembeleaka makutaniko?

  • Namna gani unaweza kupata faida wakati wanatembelea kutaniko?