Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 19

Mutumwa Muaminifu na Mwenye Busara Ni Nani?

Mutumwa Muaminifu na Mwenye Busara Ni Nani?

Chakula chetu cha kiroho kinatuletea faida sisi wote

Wakati kidogo mbele ya kifo chake, Yesu alizungumuza na wanafunzi ine kati ya wanafunzi wake, ni kusema, Petro, Yakobo, Yohana, na Andrea. Wakati huo, Yesu alitabiri juu ya alama ya kuwapo kwake mu siku za mwisho, na akauliza ulizo moja la maana. Aliuliza hivi: “Ni nani kwa kweli mutumwa muaminifu na mwenye busara mwenye bwana wake ameweka juu ya watumishi wake wa nyumbani, ili kuwapatia chakula chao kwa wakati wenye kufaa?” (Matayo 24:3, 45; Marko 13:3, 4) Yesu hakukuwa anazungumuzia chakula cha kimwili. Alilinganisha chakula na ujuzi juu ya Mungu. Yesu alihakikishia wanafunzi wake kama, kwa sababu yeye ni “bwana” wao, angeweka wale wenye wangepatia wanafunzi wake chakula mingi cha kiroho mu siku za mwisho. Ni nani wenye wangefanyiza mutumwa huyo?

Ni kikundi kidogo cha wanafunzi wa Yesu watiwa-mafuta. “Mutumwa” huyo ni Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova. Baraza hilo linatolea waabudu wa Yehova chakula cha kiroho kwa wakati wenye kufaa. Tunategemea mutumwa muaminifu ili aendelee kutupatia ‘kipimo chetu cha chakula kwa wakati wenye kufaa.’​—Luka 12:42.

Anasimamia nyumba ya Mungu. (1 Timoteo 3:15) Yesu alimupatia mutumwa huyo daraka kubwa la kusimamia kazi ya sehemu ya ku dunia ya tengenezo la Yehova, ni kusema, kutunza mali ya tengenezo, kuongoza kazi ya kuhubiri, na kutufundisha kupitia makutaniko yetu. Ili kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima kwa wakati wenye kufaa, “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anatoa chakula cha kiroho kupitia vichapo vyenye tunatumia mu mahubiri na kupitia mikutano na mikusanyiko yetu.

Mutumwa huyo ni muaminifu juu anafundisha mafundisho ya kweli ya Biblia na anatimiza mugao wake wa kuhubiri habari njema, na ni mwenye busara juu anatunza kwa hekima mali za Kristo hapa ku dunia. (Matendo 10:42) Yehova anabariki kazi ya mutumwa huyo kwa kufanya watu wengi wakuwe Mashahidi na kwa kumusaidia ili aweze kupatia watu chakula mingi sana cha kiroho.​—Isaya 60:22; 65:13.

  • Yesu aliweka nani ili apatie wanafunzi wake chakula cha kiroho?

  • Juu ya nini mutumwa ni muaminifu na mwenye busara?