Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 20

Namna Gani Baraza Lenye Kuongoza Linafanya Kazi Leo?

Namna Gani Baraza Lenye Kuongoza Linafanya Kazi Leo?

Baraza lenye kuongoza la wakati wa mitume

Barua yenye ilitumwa na baraza lenye kuongoza inasomwa

Wakati wa mitume, kikundi kidogo, ni kusema, “mitume na wazee kule Yerusalemu,” njo walifanyiza baraza lenye kuongoza, lenye lilikuwa linakamata maamuzi ya lazima kwa ajili ya kutaniko lote la Wakristo watiwa-mafuta. (Matendo 15:2) Walikuwa wanakamata uamuzi kwa umoja kwa sababu walikuwa wanachunguza kwanza mambo yenye Maandiko inasema na walikuwa wanafuata muongozo wa roho takatifu ya Mungu. (Matendo 15:25) Leo, Baraza Lenye Kuongoza linafuata mufano huo.

Mungu anatumia Baraza Lenye Kuongoza ili kufanya mapenzi yake. Ndugu watiwa-mafuta wenye kufanyiza Baraza Lenye Kuongoza wanapendezwa sana na Neno la Mungu, na wako na uzoefu sana wa kukamata maamuzi juu ya namna kazi yetu inapaswa kufanywa na juu ya mafundisho. Wanafanya mukutano kila juma ili kuzungumuzia mahitaji ya ndugu na dada mu dunia yote. Kama vile ilikuwa wakati wa mitume, Baraza Lenye Kuongoza linatoa maagizo yenye kutegemea Biblia kupitia barua ao kupitia waangalizi wenye kusafiri, na wengine. Hilo linasaidia watu wa Mungu wafikiri na kutenda kwa umoja. (Matendo 16:4, 5) Baraza Lenye Kuongoza linasimamia kazi ya kutayarisha chakula cha kiroho, linatia moyo Mashahidi wote watie kazi ya kuhubiri Ufalme pa nafasi ya kwanza, na linasimamia kazi ya kuweka ndugu kwenye madaraka mbalimbali.

Baraza Lenye Kuongoza linafuata muongozo wa roho ya Mungu. Baraza Lenye Kuongoza linategemea muongozo wa Yehova, Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi katika ulimwengu wote, na Yesu, Kichwa cha kutaniko. (1 Wakorinto 11:3; Waefeso 5:23) Ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza hawajione kuwa wao njo viongozi wa watu wa Mungu. Wao, pamoja na Wakristo wote watiwa-mafuta, “wanaendelea kumufuata Mwana-Kondoo [Yesu] kila mahali anaenda.” (Ufunuo 14:4) Ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza ni wenye shukrani sana juu ya sala zenye tunatoa kwa ajili yao.

  • Wakati wa mitume, ni nani wenye walifanyiza baraza lenye kuongoza?

  • Namna gani Baraza Lenye Kuongoza linatafuta muongozo wa Mungu leo?