Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 21

Beteli Ni Nini?

Beteli Ni Nini?

Idara Yenye Kusimamia Mambo ya Uchoraji, Inchi ya Amerika

Ujerumani

Kenya

Kolombia

Neno Beteli ni neno la Kiebrania lenye kumaanisha “Nyumba ya Mungu.” (Mwanzo 28:17, 19, maelezo ya chini) Jina hilo linafaa kwa ajili ya majengo ya biro zenye Mashahidi wa Yehova wanatumia mu dunia yote ili kuongoza na kutegemeza kazi ya kuhubiri. Baraza Lenye Kuongoza linatumikia kwenye makao yetu makubwa katika New York, Inchi ya Amerika. Wakiwa kwenye makao yetu makubwa, ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wanasimamia kazi zenye kufanywa katika biro za tawi mu inchi za mingi. Wale wenye kutumikia kwenye biro hizo, wote wanaitwa familia ya Beteli. Kama familia, wanaishi pamoja, wanatumika pamoja, wanakula pamoja, na wanajifunza Biblia pamoja katika umoja.​—Zaburi 133:1.

Ni nafasi ya pekee kwenye watu wa familia ya Beteli wanajitolea kwa kupenda. Ku kila Beteli, kuko wanaume na wanamuke Wakristo wenye wanajitoa kabisa ili kufanya mapenzi ya Mungu na kutumikia faida za Ufalme kwa wakati wote. (Matayo 6:33) Hakuna mwenye anapokeaka, lakini wote wanapewa chakula, nafasi ya kulala, na feza kidogo ili ziwasaidie kulipia mambo yao ya lazima. Ku Beteli, kila mutu iko na kazi yenye anafanyaka; wamoja wanatumikia katika biro mbalimbali, wengine wanatumikia mahali pa kupikia chakula, ao mu chumba cha kukulia chakula. Wengine wanatumikia mahali pa kuchapishia vichapo ao mahali pa kutilia vichapo jalada, mahali pa kufulia manguo, na wengine wanafanya kazi ya usafi, kazi ya kutengeneza vitu vyenye kuharibika, ao kazi zingine.

Ni nafasi kwenye kazi za mingi zinafanywa ili kutegemeza kazi ya kuhubiri Ufalme. Kusudi kubwa la kila Beteli ni kusaidia watu wengi kadiri inawezekana ili wajifunze kweli ya Biblia. Tuchukue mufano wa broshua hii: Iliandikwa chini ya usimamizi wa Baraza Lenye Kuongoza, ikatumwa kwa njia ya kielektroniki kwa vikundi mingi sana vya watafsiri mu dunia yote, ikachapwa na mashini zenye kuchapa vichapo haraka sana kwenye Beteli mbalimbali, na kisha ikatumwa mu makutaniko zaidi ya 120 000. Familia ya Beteli inasaidia katika kazi hizo zote ili kutegemeza kazi ya maana sana kuliko kazi zingine zote, ni kusema, kazi ya kuhubiri habari njema.​—Marko 13:10.

  • Ni nani wenye kutumika ku Beteli, na je, wanapokeaka?

  • Kazi yenye kufanywa ku kila Beteli iko na kusudi la kutegemeza kazi gani ya maana sana?