Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 22

Ni Kazi Gani Zinafanywa ku Biro ya Tawi?

Ni Kazi Gani Zinafanywa ku Biro ya Tawi?

Visiwa vya Salomon

Kanada

Afrika ya Kusini

Ndugu na dada wa familia ya Beteli wanafanya kazi mbalimbali ili kutegemeza kazi ya kuhubiri mu inchi moja ao zaidi. Wanaweza kufanya kazi ya kutafsiri, kuchapisha magazeti, kutia jalada ku vichapo, kutumika ku depo ya vichapo, kurekodi habari za kusikiliza tu na video, ao kufanya kazi zingine.

Halmashauri ya Tawi inasimamia kazi. Ku kila tawi, Baraza Lenye Kuongoza linaweka Halmashauri ya Tawi ili isimamie kazi. Halmashauri hiyo inafanyizwa na wazee tatu ao zaidi wenye kustahili. Halmashauri hiyo inajulisha Baraza Lenye Kuongoza namna kazi inaendelea mu kila inchi yenye inasimamia, na pia magumu yote yenye inaweza kutokea. Ripoti hizo zinasaidia Baraza Lenye Kuongoza liamue habari zenye zinapaswa kuzungumuziwa mu vichapo, ku mikutano, na mikusanyiko wakati wenye kuja. Mara kwa mara, Baraza Lenye Kuongoza linatuma wajumbe ili watembelee biro mbalimbali za tawi. Wajumbe hao wanatolea wazee wa Halmashauri za Tawi muongozo ili wafanye muzuri kazi zao. (Mezali 11:14) Mukutano wa pekee unafanywa na ku mukutano huo, mujumbe wa makao makubwa anatoa hotuba ili kutia moyo ndugu na dada wenye wanaishi mu eneo la tawi.

Halmashauri ya Tawi inategemeza makutaniko. Ndugu wenye kuwa na madaraka ku biro ya tawi wanakubali makutaniko ya mupya ianzishwe. Wanasimamia pia kazi ya mapainia, wamisionere, na waangalizi wa muzunguko wenye wanatumikia mu eneo la tawi yao. Wanafanya mipango ili mikusanyiko ya muzunguko na ya eneo ifanyike, wanasimamia kazi ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme ya mupya, na wanahakikisha kama vichapo vinatumwa mu makutaniko kupatana na mahitaji ya kila kutaniko. Kila kazi yenye inafanywa ku biro ya tawi inasaidia ili kazi ya kuhubiri ifanywe muzuri.​—1 Wakorinto 14:33, 40.

  • Namna gani Halmashauri za Tawi zinasaidia Baraza Lenye Kuongoza?

  • Ni kazi gani zinafanywa ku biro ya tawi?