Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 24

Feza Zenye Zinasaidia Kazi Yetu ya Mu Dunia Yote Iendelee Zinatokaka Wapi?

Feza Zenye Zinasaidia Kazi Yetu ya Mu Dunia Yote Iendelee Zinatokaka Wapi?

Nepali

Togo

Uingereza

Kila mwaka, tengenezo letu linachapisha na kugawia watu mamilioni ya Biblia na vichapo vingine bila kuwaomba feza. Tunajenga na kutunza Majumba ya Ufalme na majengo ya biro za tawi. Tunasaidia kutimiza mahitaji ya maelfu ya Wanabeteli na wamisionere, na tunatoa misaada wakati misiba inatokea. Kwa hiyo, pengine unaweza kujiuliza hivi: ‘Feza za kufanya ile mambo yote zinatokaka wapi?’

Hatutoe sehemu ya kumi, na hatukusanye sadaka. Hata kama tunatumia feza za mingi sana ili kutegemeza kazi yetu ya kuhubiri, hatuombe-ombe feza. Kumepita miaka zaidi ya 100 tangu gazeti la pili la Munara wa Mulinzi lilisema kama tunaamini kuwa ni Yehova njo mwenye anategemeza kazi yetu. Lilisema pia kama “hatutaomba-omba feza wala kulilia-lilia watu watoe feza,” na hatujafanya vile hata siku moja!​—Matayo 10:8.

Kazi yetu inategemezwa na michango ya kujipendea yenye watu wanatoa. Watu wengi wanapendezwa na kazi yetu ya kufundisha watu Biblia na wanatoa michango ili kuitegemeza. Mashahidi nao wanatoa kwa furaha wakati wao, nguvu zao, feza zao, na vitu vingine ili mapenzi ya Mungu ifanyike mu dunia yote. (1 Mambo ya Nyakati 29:9) Ku Jumba la Ufalme na ku mikusanyiko yetu, kuko visanduku vya michango. Kwa hiyo, wale wote wenye wanapenda kutoa michango wanaweza kuitia mu vile visanduku. Ao mutu anaweza kutoa muchango kupitia site yetu ya Enternete jw.org. Kwa kawaida, feza za mingi zenye tunapata zinatolewa na watu wenye hawako matajiri, kama ule mujane maskini mwenye Yesu alisifu juu alitia feza mbili za vichele za kidogo mu sanduku ya hazina. (Luka 21:1-4) Kwa hiyo, kila mutu anaweza ‘kuweka kitu fulani pembeni’ kwa ukawaida ili kutoa “kama vile alikusudia katika moyo wake.”​—1 Wakorinto 16:2; 2 Wakorinto 9:7.

Tuko hakika kama Yehova ataendelea kuchochea mioyo ya wale wenye wanapenda ‘kumuheshimia kupitia vitu vyao vyenye samani [ao, vya maana sana]’ ili kutegemeza kazi ya Ufalme, na kufanya mapenzi yake ifanyike.​—Mezali 3:9.

  • Ni nini inafanya tengenezo letu likuwe tofauti na dini zingine?

  • Michango ya kujipendea yenye watu wanatoa inatumiwa namna gani?