Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 25

Majumba ya Ufalme Yanajengwa Jinsi Gani na Kwa Nini?

Majumba ya Ufalme Yanajengwa Jinsi Gani na Kwa Nini?

Bolivia

Nigeria, kabla na baada

Tahiti

Kama jina lenyewe linavyoonyesha, fundisho kuu la Biblia katika majumba yetu ni Ufalme wa Mungu. Hicho ndicho kilichokuwa kichwa kikuu cha mahubiri ya Yesu.—Luka 8:1.

Ni mahali pa ibada ya kweli katika eneo. Hapo ndipo kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme huratibiwa. (Mathayo 24:14) Majumba ya Ufalme yanatofautiana kwa ukubwa na muundo, na hayana madoido. Majumba mengi hutumiwa na zaidi ya kutaniko moja. Ili kwenda sambamba na ongezeko la idadi ya makutaniko, katika miaka ya karibuni tumejenga makumi ya maelfu ya Majumba ya Ufalme (wastani wa majumba matano kila siku). Jambo hilo limewezekanaje?—Mathayo 19:26.

Yanajengwa kwa kutegemea michango. Michango hutumwa kwenye ofisi ya tawi ili makutaniko yanayohitaji kujenga au kukarabati Jumba la Ufalme yaweze kuitumia.

Hujengwa na wajitoleaji wa matabaka mbalimbali ambao hawalipwi mshahara. Katika nchi nyingi Vikundi vya Ujenzi wa Majumba ya Ufalme vimeanzishwa. Vikundi vya watumishi na wajitoleaji wa ujenzi husafiri kutoka kutaniko moja hadi jingine na wakati mwingine kwenda kwenye maeneo ambayo ni vigumu kuyafikia, ili kusaidia makutaniko kujenga Majumba ya Ufalme. Katika nchi nyingine, Mashahidi wanaostahili husimamia ujenzi na ukarabati wa Majumba ya Ufalme katika eneo walilogawiwa. Ingawa wajitoleaji wengi wenye ustadi husaidia wakati wa ujenzi, washiriki wa kutaniko hujitolea kwa wingi. Roho ya Yehova pamoja na jitihada za nafsi yote za watu wake hufanikisha kazi hiyo.—Zaburi 127:1; Wakolosai 3:23.

  • Kwa nini mahali petu pa ibada panaitwa Jumba la Ufalme?

  • Inawezekanaje kujenga Majumba ya Ufalme Ulimwenguni pote?