Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 26

Tunaweza Kusaidiaje Kudumisha Jumba Letu la Ufalme?

Tunaweza Kusaidiaje Kudumisha Jumba Letu la Ufalme?

Estonia

Zimbabwe

Mongolia

Puerto Riko

Kila Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova linawakilisha jina takatifu la Mungu. Kwa hiyo, ni pendeleo na ni sehemu muhimu ya ibada yetu takatifu kushiriki kulidumisha likiwa safi, nadhifu, na katika hali nzuri. Wote wanaweza kushiriki.

Jitolee kufanya usafi baada ya mikutano. Kila baada ya mkutano, ndugu na dada hujitolea kwa furaha kufanya usafi kwenye Jumba la Ufalme. Mara moja kila juma, usafi wa kina hufanywa. Mzee au mtumishi wa huduma hutoa maelekezo, kwa kawaida akifuata orodha ya mambo yanayopaswa kufanywa. Ikitegemea uhitaji, watu hujitolea kufagia, kusafisha sakafu, kupangusa vumbi, kupanga viti, kusafisha vyoo, kusafisha madirisha na vioo, kutupa takataka, au kufanya usafi wa nje. Angalau mara moja kwa mwaka, siku maalumu hutengwa ya kufanya usafi mkubwa. Tunapowahusisha watoto wetu kufanya usafi, tunawafundisha kuheshimu mahali petu pa ibada.—Mhubiri 5:1.

Jitolee kufanya marekebisho yanapohitajika. Kila mwaka Majumba ya Ufalme hukaguliwa nje na ndani. Kwa kutegemea ukaguzi huo marekebisho hufanywa ili kuepuka gharama zisizo za lazima baadaye. (2 Mambo ya Nyakati 24:13; 34:10) Jumba la Ufalme safi na lililotunzwa vizuri ni mahali panapofaa pa kumwabudia Mungu wetu. Tunaposhiriki katika kazi hii, tunaonyesha tunampenda Yehova na pia mahali petu pa ibada. (Zaburi 122:1) Jambo hilo linawavutia watu wengine pia katika eneo.—2 Wakorintho 6:3.

  • Kwa nini hatupaswi kupuuza mahali petu pa ibada?

  • Ni mipango gani ambayo hufanywa ili kudumisha usafi katika Jumba la Ufalme?