Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 26

Tunaweza Kufanya Nini ili Kutunza Jumba Letu la Ufalme?

Tunaweza Kufanya Nini ili Kutunza Jumba Letu la Ufalme?

Estonia

Zimbabwe

Mongolia

Porto Riko

Kila Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova liko na jina takatifu la Mungu. Kwa hiyo, tunaona kama kufanya Jumba la Ufalme liendelee kuwa safi, lenye kupendeza, na katika hali ya muzuri ni pendeleo na ni sehemu ya lazima ya ibada yetu takatifu. Sisi wote tunaweza kusaidia kufanya ile kazi.

Tujitoe ili kusafisha Jumba la Ufalme kisha mukutano. Kila siku kisha mukutano, ndugu na dada wanasafisha kwa furaha Jumba la Ufalme. Mara moja katika juma, Jumba la Ufalme linasafishwa muzuri zaidi. Muzee ao mutumishi wa huduma mumoja anasimamia ile kazi, mara mingi anatumia liste yenye kuonyesha mambo yenye inapaswa kufanywa. Kupatana na mahitaji, ndugu na dada wanajitolea ili kufagia, kukoropa, kupanguza vumbi, kupanga viti, kusafisha WC (ao musalani) na kutia ndani dawa za kuua mikrobe, kusafisha madirisha na vioo, kutupa ao kuunguza uchafu, ao kusafisha inje ya Jumba la Ufalme na kusafisha kiwanja. Mara moja hivi mu mwaka, siku fulani inapangwa ili kufanya kazi kubwa ya kusafisha Jumba la Ufalme. Tunaweza kufundisha watoto wetu waheshimie nafasi yetu ya ibada kwa kuwaomba wasaidie katika kazi fulani wakati wa kusafisha Jumba la Ufalme.​—Muhubiri 5:1.

Tujitolee ili kusaidia katika kazi ya kutengeneza Jumba la Ufalme. Kila mwaka, Jumba la Ufalme linachunguzwa inje na ndani ili kuona ikiwa kuko nafasi fulani yenye kuharibika. Uchunguzi huo unasaidia ili kazi ya kutunza Jumba la Ufalme ifanywe kwa ukawaida ili Jumba la Ufalme liendelee kuwa mu hali ya muzuri; na hilo linatusaidia tutumie feza muzuri. (2 Mambo ya Nyakati 24:13; 34:10) Jumba la Ufalme lenye kuwa safi na lenye kutunzwa muzuri ni nafasi yenye kufaa ya kumuabudia Mungu wetu. Wakati tunasaidia kutunza na kusafisha Jumba la Ufalme, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova na kama tunaheshimia kabisa nafasi yetu ya ibada. (Zaburi 122:1) Tena, Jumba la Ufalme lenye kuwa safi na lenye kutunzwa muzuri linafanya watu wa eneo letu wapendezwe na ibada yetu.​—2 Wakorinto 6:3.

  • Juu ya nini hatupaswe kuzarau nafasi yetu ya ibada?

  • Ni mipango gani yenye inafanywa ili Jumba la Ufalme liendelee kuwa safi?